Home » » MAHINDI YA ILONGA KIBOKO YA UKAME

MAHINDI YA ILONGA KIBOKO YA UKAME

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Imeandikwa na Shadrack Sagati, Lindi
WAKULIMA nchini wameshauriwa kutumia mbegu ya mahindi ya WEMA ambayo inastahimili ukame hasa kwenye maeneo yote yanayopata mvua kidogo.
Mtafiti wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga wilayani Kilosa mkoani Morogoro, alisema jana kuwa mbegu hiyo mpya inastawi kwenye udongo wenye unyevu kidogo mahindi yanastawi na kutoa mazao mengi. Mbegu hiyo imefanyiwa utafiti na watafiti wa Tanzania kuanzia mwaka 2008 na tayari kwa sasa imeshaingizwa kwenye soko la Tanzania tayari kutumiwa na wakulima.
“Lengo la kuleta mbegu hii ni kuongeza uzalishaji na usalama wa chakula,” alisema Ismail Ngolinda  kwenye Maonesho ya Nanenane yanayoendelea kwenye Viwanja vya Ngongo mjini hapa.
Alisema mbegu hiyo licha ya kustahimili ukame, lakini pia in a ukinzani dhidi ya bungua. Ngolinda aliongeza kuwa mradi wa WEMA umefanya utafiti mbegu 11 chotara ambazo zinastahimili ukame. Alisema utafiti wa mbegu hizo umefanywa kwa teknolojia ya kati.
Mtafiti huyo aliongeza kuwa mbegu hiyo inaweza kustahimili na kustawi katika maeneo yenye mwinuko kati ya mita 0 hadi mita 1,500 kutoka usawa wa bahari. “Maeneo ya Nyanda za Juu Kusini kwa kuwa kuna mwinuko mkubwa mbegu hizi hazistawi, ila maeneo mengine ya nchi mbegu hizi zinastawi,” alisema.
CHANZO HABARI LEO
 

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa