NSSF MABINGWA TAMASHA LA PASAKA 2018

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Wanamichezo kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) wakipokelewa na wenzao wa NSSF katika bandari ya Dar es Salaam baada ya kuwasili katika michezo ya tamasha la Pasaka.
Wanamichezo kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) wakipokelewa na wenzao wa NSSF katika bandari ya Dar es Salaam baada ya kuwasili katika michezo ya tamasha la Pasaka.
 Mapokezi.
Ofisa wa NSSF, Pili Mogella (kulia), akimkaribisha Ofisa wa ZSSF.  
 ZSSF wakiwasili bandarini.
 Wachezaji wa ZSSF wakiwa ndani ya basi.
Kocha wa timu ya netiboli ya NSSF, Joseph Ngánza akitoa maelekezo kwa wachezaji wake. 
 Kocha wa timu ya ZSSF, Hadia Ahmada, akitoa maelekezo kwa wachezaji wake.
Meneja wa Mahusiano na Masoko wa NSSF, Salim Kimaro, akikagua timu ya netiboli ya ZSSF.
Meneja Mahusiano na Masoko wa NSSF, Salim Kimaro akikagua timu ya netiboli ya NSSF.
 Kikosi cha timu ya ZSSF.
Kikosi cha NSSF.
Mshambuliaji wa timu ya netiboli ya ZSSF, Mwasiti Vita, akiwa katika harakati za kufunga huku Amina Jumanne (kushoto), wa NSSF akijaribu kumzuia katika mchezo wa tamasha la Pasaka uliofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
 Mchezaji wa NSSF, Maliti, akimiliki mpira huku akizongwa na mchezaji wa ZSSF, Yasinta (GD).
 Mchezaji wa timu ya netiboli ya NSSF, Fatuma Sule (C), akichuana na mchezaji wa ZSSF, Fatuma Sule (kushoto).
  Mchezaji wa timu ya netiboli ya NSSF, Fatuma Sule (C), akimiliki mpira.
 Timu ya netiboli ya NSSF wakiwa katika mazoezi.
Meneja wa Mahusiano na Masoko wa NSSF, Salim Kimaro (kulia), akizungumza na wachezaji kabla ya kuanza kwa mchezo wa netiboli ya ZSSF.
 Timu ya NSSF ikiwa mapumziko.
Mashabiki wa timu ya netiboli ya NSSF. 
 Wachezaji wa ZSSF wakiwa katika mazoezi
 Kocha wa timu ya soka ya NSFF, Sanifu Lazaro.
Zawadi za washindi.
Mshambuliaji wa NSSF, Katunguja, akimtoka Rashid Suleiman wa ZSSF (kulia).
Shaban Enzi (kulia), akichuana na Ismail Hubi wa ZSSF.
Ally Chuo wa NSSF (chini), akichuana na Rajabu Said wa ZSSF.
Wachezaji wa NSSF wakishangilia bao la pili la timu hiyo.
Mchezaji wa ZSSF, Seif Hafidh (kulia), akichuana na Said Mwinyi wa NSSF.
 Nahodha wa timu ya netiboli ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Pili Mogella, akipokea kombe la Ubingwa wa michuano ya tamasha la Pasaka kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa NSSF, Dominick Mbwete (kushoto), baada ya kuifunga ZSSF magoli 23-19  katika mchezo ulifanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dominick Mbwete (kushoto), akimkabidhi kombe nahodha wa timu ya soka ya NSSF, Mzee Mfaume, baada ya kuwafunga ZSSF mabao 2-0 katika mchezo wa tamasha la Pasaka uliofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
 Wachezaji wa timu ya soka ya NSSF wakiwa katika picha ya pamoja.
Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dominick Mbwete (kushoto), akipokea zawadi ya mlango kutoka kwa Kaimu Meneja wa Rasilimali Watu na Utawala wa ZSSF, Abdallah Mbwana.
Maofisa wa NSSF na wale wa ZSSF wakiwa katika picha ya pamoja katika bandari ya Dar es Salaam baada ya kumaliza ziara ya michezo ya tamasha la Pasaka.
Maofisa wa NSSF na wale wa ZSSF wakiwa katika picha ya pamoja katika bandari ya Dar es Salaam baada ya kumaliza ziara ya michezo ya tamasha la Pasaka.
 
TIMU ya soka ya Shirika la Taifa ya Hifadhi ya Jamii (NSSF), imeichapa bila huruma timu ya soka ya ZSSF 2-0 katika mchezo wa tamasha la Pasaka.

Mchezo huo ulifanyika mwishoni mwa wiki kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro kwa kuzikutanisha timu mbili za mashirika ya Hifadhi ya Jamii ya NSSF na ZSSF ambapo lengo la michizo hiyo ni kuimarisha ushirikiano na uhusiano baina ya mashirika hayo mawili.

Mchezo huo uliianza kwa kasi kubwa iliwachukua dakika 4 NSSF kujipatia bao la kwanza baada ya mwamuzi wa mchezo huo Fikiri Yusuph kutoa Penalti baada ya beki wa ZSSF kuunawa mpira katika harakati za kuokoa, mshambuliaji wa NSSF Said Mwinyi aliipiga penalti hiyo na kuipatia timu yake bao la kwanza.


Kuingia kwa bao hilo la mapema kuliwafanya ZSSF kucharuka na katika dakika ya 10 nusura wajipatie bao la kusawazisha baada ya shuti kali lililopigwa na Juma Mbwana kugonga mwamba na kuokolewa na walinzi wa timu ya NSSF.

ZSSF waliendelea kulisakama lango la NSSF lakini walinzi wa timu ya NSSF wamkiongozwa na beki wa wa timu hiyo Hemed Kagobe waliweza kuondoa hatari hizo na kuwapa wakati mgumu washambuliaji wa timu ya ZSSF.

Katika dakika ya 27 ya mchezo nusura ZSSF wapate bao la kusawazisha lakini golikipa wa NSSF, Sadick aliweza kuokoa kiki iliyopigwa na Rashid Suleimani na kuwa kona ambayo haikuzaa matunda.

Time hizo zilirndelea kushambuliana kea zamu hadi mapumziko NSSF ilitoka ikiwa inaongoza 1-0.

Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko ambapo ZSSF waliwatoa, Hassani Omar, Abasi Yahaya Abasi, Maulid Suleiman na Hamis Thani na nafsa zao kuchukuliwa na Yusuf Said, Abdulkarim Rajabu, Khamis Haji na Mohamed haji Khamis. 

NSSF waliwatoa Nassoro Nassor, Ally Chuo, mfungaji wa bao la kwanza Said Mwinyi, Sadick Jongo na nafasi zao kuchukuliwa na Bakari Becco, Mwinyi Mzee, Prosper Lyoba na Shaban Enzi.

Mabadiliko hayo yalibadilisha sura ya mchezo katika dakika ya 82 mshambuliaji wa timu ya NSSF, Katunguja aliifungia timu ya bao la pili banda ya kupokea pasi kutoka kwa  Mwinyi Mzee aliyeingia kipindi cha pili, kuingia kwa bao hilo kuliongeza kasi ya mchezo ambapo ZFF walikuja juu wakitaka kupata bao angalau la kufutia machozia lakini kikwazo kikubwa alikuwa mlinda mlango wa timu ya NSSF, Sadick ambaye alikuwa nyota ya mchezo kwa kuokoa mashuti yaliyokuwa yakielekezwa langoni mwake.

Wakati huohuo katika mchezo wa netiboli timu ya NSSF ilingára vilivyo baada ya kuichapa ZSSF kwa jumla ya magoli 23-19 na kunyakua kombe la michuano hiyo kwa mwaka 2018.

Akizungumza wakati akitoa zawadi kwa washindi wa michezo hiyo Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa NSSF, Dominick Mbwete, alisema kuwa michezo hii imelenga kujenga ushirikiano baina ya mifuko, kuimarisha uhusiano na pamoja na kuboresha afya kwa wadu wa michezo kupitia mifuko hiyo.

“Lengo la mashindano hayo ambayo hufanyika kila mwaka kwa kukutanisha  wanamichezo mbalimbali kutoka katika mashirika  ya ZSSF na NSSF ambapo  kushiriki kwa pamoja michezo mbalimbali pamoja na kutoa zawadi kwa wanamichezo vote walioshiriki katika tamasha hilo."

ambapo mwakani itafanyika mjini Zanzibar na kuandaliwa na ZSSF watakuwa wenyeji wa michezo hiyo Zanzib imelenga kujenga ushirikiano baina ya mifuko, kuimarisha ushirikiano baina ya ZSSF na NSSF pia imelenga kujenga ushirikiano, uhusiano baina ya wafanyakazi kutoka ZSSF pamoja na NSSF  katika kuimarisha ushirikiano.
 

MAVUNDE AIPONGEZA OSHA KWA KUBORESHA UTENDAJI WAKE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Wafanyakazi waliokingwa ipasavyo wakifanya kazi za ujenzi katika mradi wa reli ya kisasa kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro katika awamu ya kwanza ya mradi huo. OSHA huhakikisha kwamba wafanyakazi wanafanya kazi zao katika mazingira salama

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Mh. Antony Mavunde, ameupongeza Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kwa jitihada unazozichukua katika kuimarisha hali ya usalama na afya katika sehemu za kazi nchini.

Mh. Mavunde alizitoa pongezi hizo alipozungumza na wafanyakazi wa OSHA katika kikao cha pili cha baraza la tatu la watumishi hao kilichofanyika jijini Arusha mwishoni mwa wiki.

“Niwapongezi kwa kazi nzuri mnayoifanya katika kuboresha hali ya usalama na afya katika maeneo ya kazi hapa nchini. Kwakweli kumekuwa na mabadiliko makubwa sana katika utendaji wenu hasa katika kipindi cha hivi karibuni,” alisema Mh. Mavunde.

Aliongeza: “Kipindi cha nyuma mlikuwa mnafanya kazi zenu kama askari polisi jambo ambalo lilikuwa linawapa hofu kubwa wadau wenu ambao badala ya kuuelewa wajibu wao kisheria na kuutekeleza, waliishia kuwakwepa na kuwalalamikia.”

Kiongozi huyo wa serikali alieleza kwamba kwasasa watumishi wa OSHA wamekuwa wakijitahidi kufanya kazi kwa weledi mkubwa ikiwemo kuwaelimisha wadau ili waweze kuutambua wajibu wao kisheria na kuutekeleza bila kushurutishwa.

Kwa upande wake Mgeni Rasmi katika kikao hicho ambaye pia ni Katibu Mkuu (Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu), Eric Shitindi, aliwataka watumishi wa OSHA kuendelea kutekeleza majukumu yao katika namna ambayo itaboresha zaidi huduma kwa wanufaika wake.

“Kipindi cha nyuma kulikuwa na malalamiko mengi sana kutoka kwa watu tunaowahudumia lakini kwasasa malalamiko yamepungua sana. Hivyo nawaomba muendelee kutoa huduma nzuri kwa wateja wenu kwa kuzingia vyema Sheria na Kanuni mbali mbali zilizopo,” alisema mgeni rasmi.

Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala, Khadija Mwenda, alisema kikao hicho cha baraza la wafanyakazi kinalenga kufanya tathmini ya utendaji wa taasisi kwa kipindi kilichopita na kuweka mikakati ya kujiimarisha zaidi kiutendaji kwa kipindi kijacho.

Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) ni taasisi ya serikali yenye dhamana ya kusimamia masuala ya Usalama na Afya za wafanyakazi wanapokuwa katika sehemu zao za kazi. Wakala hufanya kaguzi za kiusalama na afya katika sehemu zote za kazi hapa nchini. OSHA pia huwashauri wamiliki ama wasimamizi wa maeneo ya kazi juu ya uwekaji na usimamizi wa mifumo ya kulinda afya na usalama wa wafanyakazi wanapokuwa kazini.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Rodney Thadeus akizungumza na Maafisa Habari na Mawasiliano kutoka katika Halmashauri na Mikoa ya Morogoro, Manyara, Dodoma, Kilimanjaro na Tanga yaliyofunguliwa jana jumanne Machi 20, 2018. Mafunzo hayo ya siku nne yamendaliwa na Mradi na Uimarishaji Mifumo ya Sekta ya Umma (PS3) kwa kushirilkiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa mna Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kupitia ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID).
Mwezeshaji na Afisa Habari kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Nteghenjwa Hosseah akiwasilisha mada kuhusu mtindo wa uandishi wa habari katika tovuti kutoka katika Halmashauri na Mikoa ya Morogoro, Manyara, Dodoma, Kilimanjaro na Tanga yaliyofunguliwa jana Jumanne Machi 20, 2018. Mafunzo hayo ya siku nne yamendaliwa na Mradi na Uimarishaji Mifumo ya Sekta ya Umma (PS3) kwa kushirilkiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa mna Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kupitia ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID).

Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya uandishi wa habari za tovuti kutoka katika Halmashauri na Mikoa ya Morogoro, Manyara, Dodoma, Kilimanjaro na Tanga wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa mafunzo hayo yaliyofunguliwa jana Jumanne Machi 20, 2018 Mkoani Morogoro. Mafunzo hayo ya siku nne yamendaliwa na Mradi na Uimarishaji Mifumo ya Sekta ya Umma (PS3) kwa kushirilkiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa mna Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kupitia ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID)
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya uandishi wa habari za tovuti kutoka katika Mikoa na Halmashauri mbalimbali nchini wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa mafunzo hayo yaliyofunguliwa jana Jumanne Machi 20, 2018 Mkoani Morogoro. Mafunzo hayo ya siku nne yamendaliwa na Mradi na Uimarishaji Mifumo ya Sekta ya Umma (PS3) kwa kushirilkiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa mna Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kupitia ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID).
Afisa Tehama kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro, Alfred Chali akichangia hoja wakati wa mafunzo ya uandishi wa habari za tovuti kutoka katika Halmashauri na Mikoa ya Morogoro, Manyara, Dodoma, Kilimanjaro na Tanga yaliyofunguliwa jana Jumanne Machi 20, 2018. Mafunzo hayo ya siku nne yamendaliwa na Mradi na Uimarishaji Mifumo ya Sekta ya Umma (PS3) kwa kushirilkiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa mna Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kupitia ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID).

MAAFISA Habari na Mawasiliano katika Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini wametakiwa kuacha kufungia katika makabati na makabrasha taarifa chanya za utekelezaji wa mikakati, miradi na programu mbalimbali za Serikali na badala yake watangaze mafanikio hayo kwa umma.

Hayo yamesemwa jana (Jumanne Machi 20, 2018) Mkoani Morogoro na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Rodney Thadeus wakati wa ufunguzi wa mafunzo kuhusu mwongozo wa uandishi wa habari za tovuti kupitia Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) unaofadhiliwa na Shirika la Misaada la Marekani (USAID).

Thadeus alisema Serikali inatekeleza miradi mikubwa ya maendeleo katika Mikoa na Halmashauri mbalimbali nchini, hivyo ni wajibu wa Maafisa Habari na Mawasiliano katika maeneo hayo watangaze mafaniko hayo badala ya kusubiri maswali na hoja mbalimbali za wananchi wakihoji katika kupata uelewa kuhusu miradi hiyo.

“Maafisa Habari, msifungie taarifa katika makabati yenu toeni taarifa kwa Umma, wananchi wanapenda kufahamu nini kinafanywa na Serikali yao hivyo jukumu la Afisa Habari ni kupiga picha kuandaa taarifa na wekeni vielelezo hivyo katika tovuti zenu ili kujibu hoja za wananchi” alisema Thadeus.

Aidha, alisema ni wajibu wa Maafisa Habari na Mawasiliano kuhakikisha kuwa wanaweza taarifa mpya kila wakati ili kuhakikisha kuwa zinakidhi mahitaji ya msingi ya wananchi ambao wamekuwa wakitumia muda mrefu kwa ajili ya kutafuta huduma mbalimbali zinazotolewa na Serikali katika maeneo yao ya kazi.

Akifafanua zaidi alisema Maafisa Habari na Mawasiliano katika Mikoa na Halmashauri mbalimbali nchini ndiyo wataalamu wa masuala ya Mawasiliano katika maeneo yao ya kazi, hivyo wana wajibu wa kutoa ushauri kwa viongozi wao wa kazi kwa ajili ya kutoa ufafanuzi wa mara kwa mara kuhusu hoja mbalimbali zinazoulizwa na kujitolea majibu kwa wakati.

Aliongeza kuwa matumizi ya tovuti ndiyo njia ya haraka zaidi ya kurahisisha mfumo wa utoaji wa habari na taarifa mbalimbali za Halmashaauri na Mikoa, hivyo ni wajibu wa Maafisa Habari na Mawasiliano kuwa mabalozi ili kuhakikisha kunakuwepo na daraja la mawasiliano baina ya Serikali na wananchi katika kupata suluhu ya masuala mbalimbali ikiwemo migogoro inayotokea mara kwa mara.

Kwa upande wake, Kiongozi wa Timu ya Utawala Bora kutoka PS3, Dkt. Peter Kilima alisema uboreshaji wa tovuti ni sehemu muhimu ya utekelezaji wa dhana halisi ya utawala bora hivyo ni wajibu wa Maafisa Habari na Mawasiliano katika Mikoa na Halmashauri nchini kuhakikisha kuwa wananchi wanapata taarifa zinazozingatia muda na mahitaji yaliyopo.

Aliongeza ni wajibu wa Maafisa Habari na Mawasiliano kuzingatia mafunzo kuhusu mwongozo wa uandishi wa habari katika tovuti za Serikali katika Mikoa na Halmashauri mbalimbali nchini kwa kuwa wananchi wana matarajio makubwa na Serikali yao katika kuwapatia huduma mbalimbali.

WANAFUNZI MVOMERO WATAKIWA KUJIKITA ZAIDI KATIKA MASOMO YA SAYANSI ILI WAWE WATAFITI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mohamed Utalli, akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Milama, iliyopo mkoani Morogoro baada ya kukabidhi mbegu bora ya mahindi ya Wema 2109 kwa ajili ya shamba darasa. Makabidhiano hayo yamefanyika wilayani humo leo.
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Shabani Hussein (wa pili kulia), akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mohamed Utalli (katikati) mbegu ya Wema 2109 kwa ajili ya kuwakabidhi wakulima wa wilaya yake ili waanzishe mashamba darasa. Wengine kutoka kushoto ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Mvomero, Hilali Focus Riddy, Ofisa Kilimo wa Wilaya ya Mvomero, Daina Muywanga na kulia ni Mtifiti Kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga mkoani Morogoro, Mikidadi Hamidu.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi, Mvomero wakiandaa shamba kwa ajili ya kupanda mbegu ya Wema katika shamba darasa.
Ofisa mradi huo kutoka COSTECH, Bestina Daniel (kushoto), akizungumza katika uzinduzi wa shamba darasa katika Shule ya Msingi Mvomero.
Uzinduzi ukiendelea.
Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, akizungumza wakati wa uzinduzi wa shamba darasa katika Shule ya Msingi Mvomero.
Wanafunzi wa shule hiyo wakikabidhiwa mbegu hiyo ya Wema.
Mkulima Yacob Patrick, akikabidhiwa mbegu hiyo.
Mkulima Mohamed Maungo, akikabidhiwa mbegu.
Mkulima Tatu Mbonde, akikabidhiwa mbegu.
Walimu wa Shule ya Msingi Mvomero wakikabidhiwa mbegu.
Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mohamed Utalli, akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi Mvomero.
Mtifiti Kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga mkoani Morogoro, Mikidadi Hamidu ambao ndio waliofanya utafiti wa mbegu hiyo, akitoa maelezo ya jinsi ya kupanda mbegu hiyo.
Uzinduzi wa shamba darasa katika shule ya msingi Mvomero.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mvomero wakiwa katika upandaji wa mbegu hizo.
Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mohamed Utalli akizindua shamba darasa kwa kupanda mbegu hiyo ya Wema 2109
Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mohamed Utalli, akizungumza na wakulima wanaounda kikundi cha Tupendane kilichopo Kijiji cha Didamba.
Mwenyekiti wa Kikundi cha Tupendane cha Kijiji cha Didamba, Mwanahamisi Omari (kushoto), akikabidhiwa mbegu.
Mkulima Maulid Adamu kutoka Kikundi cha Kazibanza kilichopo Kijiji cha Milama akikabidhiwa mbegu.


Na Dotto Mwaibale, Mvomero-Morogoro.

WANAFUNZI wa Shule ya Msingi ya Mvomero mkoani Morogoro wametakiwa kujikita zaidi katika masomo ya Sayansi ili waweze kulisaidia taifa katika nyanja mbalimbali ikiwemo kufanya utafiti.

Mwito huo umetolewa wilayani humo leo na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Shabani Hussein wakati wa uzinduzi wa shamba darasa la mbegu ya mahindi ya Wema E2109 inayostahimili ukame iliyotolewa na COSTECH kupitia Jukwaa na Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB)

"Ninyi wanafunzi nawaomba someni sana masomo ya sayansi ili hapo baadae muweze kuwa watafiti wa masuala mbalimbali jambo litakalosaidia taifa" alisema Hussein.Alisema tafiti zozote zinafanywa na wataalamu waliobobea katika masomo sayansi hivyo aliwataka wanafunzi hao kujifunza kwa bidii masomo hayo ya sayansi.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mkuu wa Wilaya hiyo, Mohamed Utalli aliishukuru COSTECH na OFAB kwa kupeleka mradi huo katika wilaya yake ambapo amewataka wananchi kuzichangamkia mbegu hizo.

"Tuna bahati sana katika mkoa wetu kwani katika mikoa tisa ambayo mradi huo utafanyika na sisi tupo hivyo ni fursa kwetu tusiiache ikapotea bure" alisema Utalli.Utalli aliwataka wakulima wilayani humo ulimopita mradira huo kuhakikisha wanayatunza mashamba hayo ili kuleta tija katika zao la mahindi.

Alisema mradi huo ni utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuunga mkono jitihada za Rais John Magufuli za kufanya kazi kwa bidii wakati taifa likiingia katika uchumi wa kati wa viwanda.

Akizungumza wakati wa kukabidhi mbegu hizo, Ofisa mradi huo kutoka COSTECH, Bestina Daniel alisema kazi kubwa ya COSTECH ni kuishauri serikali katika masuala yote yanayohusu Sayansi na Teknolojia na kusimamia tafiti zote za kisayansi katika maeneo mbalimbali na kilimo na kuhakikisha zinawafikia walengwa ambao ni wakulima.

Alisema mbegu hizo walizozikabidhi zimefanyiwa utafiti na zitapandwa katika mashamba darasa na baadae kusambazwa kwa wakulima wengine ili kuondoa changamoto ya kukosekana kwa mbegu bora kutokana na wakulima kukabiliwa na mbegu ambazo zilikuwa hazina ubora.

Mtifiti Kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga mkoani Morogoro, Mikidadi Hamidu alisema iwapo mkulima atafuata ushauri wa upandaji wa mbegu hiyo ya Wema 2109 katika ekari moja atapata magunia 35 tofauti na mbegu nyingine ambapo wanapata chini ya hapo.

Aliongeza kuwa mbegu hiyo italeta matokeo mazuri iwapo kanuni za kilimo bora zitafuatwa kama vile kufuata vipimo, maandalizi ya shamba, matumizi ya mbolea zote ya kupandia na kukuzia na kuwa mbegu hiyo ni moja kati ya mbegu 11 zilizofanyiwa utafiti.
 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa