Home » » NSSF YASHIRIKI MAONYESHO YA NANENANE MKOANI MOROGORO

NSSF YASHIRIKI MAONYESHO YA NANENANE MKOANI MOROGORO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Afisa wa NSSF Mr Shaban Salehe akimwandikisha mwanachama mpya katika banda la NSSF katika maonyesho ya Nanenane yanayoendelea mkoani Morogoro.
Afisa wa NSSF, Mwanawetu Njozi (kulia) akiongea na mgeni alietembelea banda la NSSF katika maonyesho ya Nanenane yanayoendelea mkoani Morogoro.
Afisa wa NSSF, Jonathan Mkahala akimwandikisha mwanachama mpya katika banda la NSSF katika maonyesho ya Nanenane yanayoendelea mkoani Morogoro, Pembeni kushoto ni Afisa mwandamizi wa Matekelezo wa Shirika hilo, Bw. Salawa.
Afisa Mwandamizi wa Masoko na Uhusiano, Amina Mbaga akizungumza na wageni walietembelea banda la NSSF katika maonyesho ya Nanenane yanayoendelea mkoani Morogoro.

Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) linashiriki maonyesho ya Kilimo yanayoendelea mkoani Morogoro, Katika maonyesho hayo wakazi wote wa Morogoro Hususan Wakulima wanakaribishwa kupata elimu kuhusu namna ya kushiriki kilimo cha miwa (Outgrowers Scheme) Mpango huu umeanziishwa mahususi ili kuwasaidia watanzania kupata kipato kwa kulima miwa na Miwa hiyo itanunuliwa moja kwa moja na Kampuni Hodhi ya Mkulazi ambayo ni ubia kati ya NSSF na PPF. 

Vile vile wananchi wote wanakaribishwa kujiandikisha na NSSF ili kupata Matibabu bure kwa mwanachama na wategemezi wake pamoja na Mafao mengine yatolewayo na NSSF kama vile Mafao ya uzazi, kuumia kazini, Mafao ya urithi, Pensheni ya uzeeni na mengineyo

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa