Home »
» WAZIRI WA UTAMADUNI NA SANAA WA AFRIKA YA KUSINI ATEMBELEA MAZIMBU CAMPUS MKOANI MOROGORO NA KUTEMBELEA MAKABURI YA WAPIGANIA UHURU WA AFRIKA YA KUSINI.
WAZIRI WA UTAMADUNI NA SANAA WA AFRIKA YA KUSINI ATEMBELEA MAZIMBU CAMPUS MKOANI MOROGORO NA KUTEMBELEA MAKABURI YA WAPIGANIA UHURU WA AFRIKA YA KUSINI.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
|
Waziri wa Utamaduni
na Sanaa wa Afrika ya Kusini Mhe. Nathi Mthethwa akisalimiana na Mkurugenzi wa SUA
Solomon Mazimbu Campus Prof.Yasinta Muzanila alipowasili kutembelea eneo lililopo
Mkoani Morogoro ambalo wapigania uhuru wa Afrika ya Kusini walilitumia katika
harakati za kupigania uhuru wao na ukombozi wa bara la Afrika kwa ujumla.
|
|
Mkurugenzi wa SUA
Solomon Mazimbu Campus Prof.Yasinta Muzanila(kulia) akitoa maelezo kwa Waziri
wa Utamaduni na Sanaa wa Afrika ya Kusini Mhe. Nathi Mthethwa(kushoto) kuhusu
Mazimbu campus na kumbukumbu zilizopo wakati
Waziri huyo alipotembelea eneo hilo liliopo Mkoani Morogoro ambalo wapigania
uhuru wa Afrika ya Kusini walilitumia katika harakati za kupigania uhuru wao na
ukombozi wa bara la Afrika kwa ujumla.
|
|
Waziri wa Utamaduni
na Sanaa wa Afrika ya Kusini Mhe. Nathi Mthethwa (aliyenyoosha mkono)
akiangalia moja ya makaburi ya waliopigania uhuru wa nchi yake yaliyopo Mazimbu
Campus Mkoani Morogoro.
|
|
Waziri wa Utamaduni
na Sanaa wa Afrika ya Kusini Mhe. Nathi Mthethwa akiwa katika eneo lililowekwa
sanamu ya Rais wa kwanza Afrika ya Kusini Hayati Nelson Mandela kama ukumbusho
wa wapigania uhuru wa Afrika ya Kusini Mazimbu Mkoani Morogoro.
|
|
Waziri wa Utamaduni
na Sanaa wa Afrika ya Kusini Mhe. Nathi Mthethwa akiangalia mti uliopandwa na
moja wa viongozi wa Afrika Kusini kama kumbukumbu kwa wapigania uhuru wa Afrika ya Kusini Mazimbu
Campus Mkoani Morogoro.
|
|
Waziri wa Utamaduni
na Sanaa wa Afrika ya Kusini Mhe. Nathi Mthethwa akiweka shada la maua kwenye
mnara wa kumbukumbu ya makaburi ya waliopigania uhuru wa Afrika ya Kusini
yaliyopo Mazimbu Mkoani Morogoro.
|
|
Moja ya alama zilizowekwa na mmoja wa viongozi
wa Chama cha ANC Bw. Oliver Tambo ikiwa ni
kumbukumbu ya mashujaa ya waliopigania uhuru wa Afrika ya Kusini. |
|
Waziri wa Utamaduni na Sanaa wa Afrika ya Kusini
Mhe. Nathi Mthethwa akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa Mazimbu Campus
na ujumbe kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo wakati
alipotembelea eneo hilo katika ziara yake hapa nchini. |
0 comments:
Post a Comment