Na Ally Daud-MAELEZO
MOROGORO.
WATANZANIA
hasa watumiaji Wa pombe na Uvutaji Sigara wamehaswa kuepuka matumizi
hayo kwani yanachangia kuongeza magonjwa yasiyoambukiza ili kusaidia
kupunguza asilimia 1.5 ya vifo vinavyotokana na magonjwa hayo kwa
kukinga, kutibu na kuzingatia afya ya akili kufikia mwaka 2030.
Akizungumza
hayo kwenye ufunguzi Wa mkutano Wa Utekelezaji Wa mpango mkakakti na
Huduma za magonjwa yasiyoambukiza kwa madaktari na watoa huduma za afya
ngazi ya mkoa na wilaya Mkurugenzi wa Tiba Wizara ya Afya , Maendeleo
ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Magreth Mhando Mkoani Morogoro.
"Watanzania
wanatakiwa kuepuka matumizi ya unywaji pombe na uvutaji wa Sigara kwa
wingi ili kuepuka magonjwa yasioambukizwa na kutokomeza vifo
vinavyosababishwa na magonjwa hayo ili kujenga taifa lenye afya imara na
uchumi mzuri" alisema Dkt. Mhando
Aidha
Dkt. Mhando amesema kuwa idadi ya watu wanaotumia pombe imefikia
asilimi 29.3 na wanaovuta sigara imefikia asilimia 15.9 , wenye uzito
kupita kiasi asilimia 34.7 ikiwa imeongeza idadi ya wagonjwa wa
shinikizo la damu kwa asilimia 25.9 na kisukari asilimia 9.1 kutoka
asilimia moja mwaka 2012.
Mbali
na hayo Dkt. Mhando amesema kuwa malengo ya mkutano huo ni kuhakikisha
wanapata ufumbuzi wa kina na kuadhimia kupunguza nusu ya vifo
vinavyotokana na ajari za barabarani nchini kufikia 2020 ili kutimiza
mpango wa maendeleo wa SDG mwaka 2030 .
Kwa
upande wake Kaimu Mkurugenzi msaidizi wa magonjwa yasioambukizwa
Shadrack Buswelu amesema kuwa watanzania wanatakiwa kuepuka ulaji
usiokua na tija na wajikite kwenye mazoezi ya mara kwa mara ili kuepuka
magonjwa yasioambukiza na kujenga taifa lenye watu shupavu kwa
maendeleo ya nchi.
“Watanzania
tunatakiwa kuepuka ulaji usio na tija na tufanye mazoezi ya mara kwa
mara ili kuepuka magonjwa yasioambukiza na kujenga taifa lenye watu
imara kwa maendeleo yetu” alisema Bw. Buswelu.
Mkutano
huo wa siku tatu unahudhuriwa na watoa huduma za afya ngazi ya mkoa na
wilaya pamoja na taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali unalenga
kuweka mkakati wa kupambana na magonjwa yasioambukiza kama vile kisukari
, shinikizo la damu, uzito kuzidi kiasi na ajari za barabarani mpaka
kufikia 2020.
0 comments:
Post a Comment