Home » » ‘Boresheni maslahi ya wafanyakazi wenu’

‘Boresheni maslahi ya wafanyakazi wenu’

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Askofu Thelesphor Mkude wa Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro
WAAJIRI nchini wameaswa kutafuta njia za kuboresha maslahi kwa wafanyakazi wao, badala ya kuwalipa mshahara mdogo kwa kuendekeza maslahi binafsi.
Rai hiyo ilitolewa na Askofu Thelesphor Mkude wa Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro, baada ya kufungua mkutano mkuu wa nne wa Chama cha wafanyakazi Wakatoliki Tanzania (CWM), uliofanyika katika parokia ya roho mtakatifu kiwanja cha ndege Mjini hapa.
Alisema licha ya wafanyakazi kutumia juhudi zao katika kazi mbalimbali, baadhi ya waajiri huwalipa mshahara mdogo na wakati mwingine kuwacheleweshea.
Aidha, alisema waajiri watafute upeo na utajiri wao lakini wasisahau kuwa wafanyakazi wao wanapaswa kulipwa inavyostahili kadri ya mapatano yao na kwamba lazima mapatano hayo yalingane na kima cha serikali.
Alisema kila mtu anapenda kufanya kazi ili apate mapto tena halali ambapo. Alieleza kuwa baadhi ya waajiri wanapenda kuwanyonya wafanyakazi wao kwa kutowalipa mishahara wanayostahili.
“Haiwezekani mtu mmoja akajitayarisha kwa kuwanyonya wengine kwa kutowalipa mishahara wanayostahili, ni bora kama hawezi afunge kiwanda chake,”alisema Mkude Alisema kuwa wengine wanapotaka kupata faida huwa hawaangalii njia ya kupata faida.
Chanzo Na Habari Leo

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa