Home » » Wilaya yakosa ofisi ya TRA miaka 13 mfulilizo.

Wilaya yakosa ofisi ya TRA miaka 13 mfulilizo.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 



Na Godfriend Mbuya

Wilaya ya Kilindi Mkoani Tanga haina Ofisi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) jambo ambalo linasababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi wa wilaya hiyo wanapohitaji huduma mbalimbali zinazohitaji kuwezeshwa na TRA.

Akizungumza Bungeni Mjini Dodoma wakati akiuliza swali kwa serikali Mbunge wa Kilindi Omary Kigua (CCM) aliyetaka kujua ni lini serikali itafungua ofisi ya wilaya ili wananchi waweze kulipa mapato kwa urahisi kuliko ilivyo sasa.

Akijibu sali hilo Naibu Waziri wa Fedha Bi. Ashanti Kijaji amesema serikali inatambua umuhimu huo wa kuanzisha ofisi hiyo lakini kwa sasa kipaumbele kipo katika mikoa mipya iliyoanzishwa.

Aidha naibu Waziri amewataka wananchi wa Kilindi kuendelea kulipa kodi wakati serikali ikiendelea na mchakato wa kufanya upembuzi wa kubaini gharama za kuanzisha ofisi hiyo na vyanzo vitakavyo changia kuongeza mapato wilayani Kilindi.

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa