Home » » Liyumba kuzikwa Mahenge

Liyumba kuzikwa Mahenge

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsappnamba +255765056399.


MWILI wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba aliyefariki juzi jijini Dar es Salaam unatarajiwa kusafirishwa kwenda kuzikwa kijijini kwake Mahenge mkoani Morogoro.
Liyumba alifariki dunia juzi saa 10 jioni katika Hospitali ya Agha Khan jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu ya maradhi ya kisukari na shinikizo la damu.
Akizungumza na gazeti hili jana, Msemaji wa familia hiyo, Moses Liyumba alisema mipango ya mazishi inaendelea kufanyika nyumbani kwa marehemu maeneo ya Triple Seven, Mikocheni, Dar es Salaam na huenda leo au kesho mwili wa marehemu ukasafirishwa kwenda kijiji cha Vigoi kwa maziko.
“Tunaendelea na taratibu mbalimbali za mazishi na huenda mambo yakienda sawa kesho (leo) au kesho kutwa tukausafirisha mwili wa marehemu hadi kijijini kwake kwa maziko,” alisema Liyumba.
Kwa mujibu msemaji huyo wa familia, marehemu ameacha watoto wanane ambao walizaliwa na mama tofauti kati yao wa kike sita na wa kiume wawili.

 Chanzo Gazeti la Habari leo

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa