Home » » HABARI NJEMA: MTANDAO WA KASI WA SMILE WAWAFIKIA WAKAZI WA MOROGORO

HABARI NJEMA: MTANDAO WA KASI WA SMILE WAWAFIKIA WAKAZI WA MOROGORO



Kampuni ya mawasiliano ya Smile Tanzania leo imezindua huduma zake za mtandao wake wa kasi kwa matumizi ya binafsi,wafanya biashara waliopo ndani na jirani na Mkoa wa Morogoro.
Akizungumza wakati wa hafla fupi ya uzinduzi mkoani Morogoro, Meneja Mkaazi wa Kampuni ya Mawasiliano ya Smile Tanzania, Bw. Eric Behner amebainisha kuwa kampuni yake inatoa huduma zenye kasi zaidi na kuaminika kwa wateja wake nchini Tanzania kupitia mtandao wa 4G LTE kwenye wigo wa 800MHz yenye kasi ya kufikia mpaka 21Mbps.
“Smile imetumia tekinolojia na viwango vya hali ya juu vya mawasiliano vilivyopo katika kutimiza ahadi yake ya kutoa vifurushi vya intaneti vyenye kasi ya aina yake, ubora mkubwa, mtandao wa kuaminika unaotumia vifaa rahisi kutumia na kufanya mapinduzi makubwa ya namna watu wanavyoweza kuzifikia huduma za intaneti.” Alisema Bw. Behner
“Tunayo furaha kubwa kuleta tekinolojia ya mtandao wa kisasa kwa wakazi wandani na jirani mkoaniMbeya.Tuna uhakika wa kwamba upatikanaji wa intaneti yenye kasi utasaidia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya kibiashara na watu binafsi hapa mkaoni na nifaraj kubwa kwetu kuwa sasa kila mtu hapa Mbeya sasa atajionea na kujivunia mwenyewe mtandao huu kuwa ni wa uhakika na wenye huduma za gharama nafuu.” Aliongezea Bw. Behner
Kampuni ya Smile pia imeleta huduma ambayo itakuwa ni msaada mkubwa kwa wafanya biashara wa mkoani Mbeya, ambapo kutakuwa na kiungio maalumu cha wigo mpana wa mtandao na kuyawezesha makampuni yenye upungufu wa kuwasiliana na wafanyakazi ambao wako nje ya ofisi kwa sababu moja au nyingine, basi itawaongezea uwezo wa kuzalisha na kupunguza gharama za uendeshaji. 
Katika sekta ya mawasiliano nchini Tanzania hivi sasa huduma ya mtandao wa intaneti ya Smile ndiyo inayoongoza kwa kuwa na kasi ambayo ni mara kumi zaidi ya ile ya 3G.Wateja sasa watajionea intaneti yenye kasi zaidi, hususani wakati wa kupakia mafaili makubwa, kutuma barua pepe zenye viambatanisho vikubwa, pamoja na kupakua mafaili, muziki, filamu na michezo ya mtandaoni. Vilevile kupata huduma mbalimbali za kimtandao kama vile; kwa kutazama video au luninga mtandaoni bila ya kukwama au kufunguka kwa muda mrefu.

“Tunajivunia kwa kweli kuwaletea huduma ya intaneti yenye kasi zaidi mkoani Mbeya ambayo ni sawa na ile yenye kasi na ubora wanayoifurahia wenzetu wa Ulaya. Smile hatutoi huduma ya intaneti pekee, bali tutatoa huduma ya intaneti yenye kasi zaidi, kuaminika wakati wote na yenye gharama ambayo kila mtu ataweza kuimudu na pia tumejizatiti katika kuwaridhisha wateja wetu kwa kiwango cha hali ya juu.” Alisisitiza Bw. Behner
Mikoa mingine ambayo tayari huduma ya Smile zinapatikana na inatarajiwa kunufaika na huduma hizi ni Dar Es Salaam,Mwanza,Mbeya,Arusha,Kilimanjaro naDodoma.Smile inatarajia kuendelea kujipanua kwenye mikoa mingine  Katika huduma za 4G LTE.
Baada ya uzinduzi huo, kampuni ya mawasiliano ya Smile Tanzania imewataka wakazi wa mkoani Morogorona maeneo ya jirani kutembelea duka lao li kujaribu na kushuhudia kasi ya mtandao huo ulio wa ajabu au kuwasiliana na kitengo cha huduma kwa wateja kwa kupiga simu namba 0662 100 100.

Imetolewa na;
Linda Chiza
Smile Communications Tanzania




Kwa niaba ya:
Smile Communications Tanzania www.smile.co.tz
 

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa