Home » » LENGO NI KUWAWEZESHA KUFANYA BIASHARA ZAO KWA TIJA

LENGO NI KUWAWEZESHA KUFANYA BIASHARA ZAO KWA TIJA

  Wakazi wa jiji la Tanga wakichagua maembe katika Soko la Masiwani Chuma, matunda hayo husafirishwa kutoka kutoka Mombasa na kupelekwa katika mikoa mbalimbali kutafuta masoko.
Halmashahuri ya Manispaa ya Morogoro, kwa kushirikiana na Chuo cha Ufundi Stadi (Veta), inakusudia kuanzisha mpango maalumu wa elimu kwa wajasiriamali wadogo wenye lengo la kuwawezesha kupata maarifa ya kuendesha biashara zao kwa tija.
Elimu hiyo pia inalenga kuwawezesha washiriki kujua mbinu za kupata mitaji kutoka katika taasisi mbalimbali za fedha.
Hayo yalisemwa jana na meya wa Manispaa ya Morogoro, Amir Nondo alipokuwa akizungumza na wanachama wa kikundi cha Vikoba Mshikamamo ‘B’.
Nondo alisema mpango huo umekuja baada ya kubainika kuwa wajasiriamali wengi wanafanya biashara zao bila elimu ya biashara, hali inayowafanya washindwe kupiga hatua.
Meya huyo alisema elimu ya biashara inahitajika kwa wajasiriamali hasa katika kipindi hiki ambacho kina ushindani mkubwa wa bidhaa sokoni.
“Ndiyo maana tumeamua kuwasaidia wajasiriamali kupata elimu nao waendeshe biashara zao kwa umakini zaidi kuliko ilivyo sasa,” alisema.
Kwa upande wake, mwenyekiti wa Vikoba Mshikamano ‘B’, Sauda Juma alisema wanachama wake wanakabiliwa na changamoto mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kikundi kutokuwa na mtaji wa kutosha kuweza kukopeshana kiwango kikubwa cha fedha.
“Hii ni changamoto inayotusumbua, tunawaomba wadau wajitokeze kutusaidia kukuza mtaji wetu,” alisema.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa