Home » » WAJUMBE IDARA YA UTUMISHI WA WALIMU WATEMBELEA NYUMBA ZA PSPF LUKOMBE, MOROGORO

WAJUMBE IDARA YA UTUMISHI WA WALIMU WATEMBELEA NYUMBA ZA PSPF LUKOMBE, MOROGORO


Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Neema Muro, (Kushoto), akizungumza na baadhi ya wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu, kwenye eneo la mradi wa nyumba za Mfuko huo eneo la Lukobe mjini Morogoro mwishoni mwa wiki. Wajumbe hao walifanya ziara hiyo mara baada yab kuhudhuria semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mfuko huo kwa lengo la kuwaelimisha juu ya faida mwanachama anazoweza kupata anapojiunga na Mfuko huo.
Mkurugenzi wa uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Neema Muro, (Kushoto), akiwapa maelezo, baadhi ya wajumbe wa tume ya utumishi wa walimu, kuhusu mradi wa nyumba za Mfuko huo, zilizoko eneo la Lukobe mjini Morogoro, mwishoni mwa wiki.
Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Abdul Njaidi, (Mwenye T-Shirt), akiwapa maelezo wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu, kuhusu nyumba za Mfuko huo zilizoko eneo la Lukobe mjini Morogoro, mwishoni mwa wiki mara baada ya kuhudhuria semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mfuko huo mjini humo.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa