Home » » mkutano wa masuala ya madini wafanyika mjini Morogoro

mkutano wa masuala ya madini wafanyika mjini Morogoro

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kamishna wa Madini, Mhandisi Paul Masanja (kushoto) akieleza jambo kabla ya ufunguzi wa Kikao cha Kazi cha Idara ya Madini. Katikati ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Bw. Alfred Shayo ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika kikao hicho.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Bw. Alfred Shayo (katikati) akifungua rasmi kikao cha Kazi cha Idara ya Madini kilichofanyika hivi karibuni katika hoteli ya Kings Way ya Mkoani Morogoro. Kushoto ni Kamishna wa Madini, Mhandisi Paul Masanja na kulia ni Kamishna Msaidizi wa Madini- Uratibu, Mhandisi John Shija.

Baadhi ya wajumbe walioshiriki katika kikao cha kazi cha Idara ya Madini wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa katika kikao hicho.
Kamishna wa Madini, Mhandisi Paul Masanja (kushoto) akimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Bw. Alfred Shayo wakati wa ufunguzi wa kikao cha kazi cha Idara ya Madini kinachofanyika katika hoteli ya King’s Way ya Mkoani Morogoro.
Kamishna wa Madini, Mhandisi Paul Masanja (wanne kutoka kushoto, waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa kikao cha kazi cha Idara ya Madini kilichofanyika hivi karibuni katika Hoteli ya Kings Way ya Mkoani Morogoro. Kushoto kwake ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Bw. Alfred Shayo ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika kikao hicho.

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa