Home » » VIJANA MIKUMI WATAKIWA KUACHANA NA UJANGILI

VIJANA MIKUMI WATAKIWA KUACHANA NA UJANGILI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

VIJANA kutoka vijiji 20 vinavyozunguka hifadhi ya taifa ya Mikumi Kilosa mkoani Morogoro wameshauriwa kuacha mara  moja kujihusisha na vitendo vya ujangili na badala yake kuunda  vikundi vidogo vya ujasiriamali ili wapewe fursa za mikopo.
Rai hiyo imetolewa juzi na Mbunge wa Mikumi, Abdusalaam Sas,  wakati akizindua tamasha la kupiga vita ujangili na mauaji ya  tembo, lililoandaliwa na mtandao wa habari za kijamii Tanzania  (Mhakita), chini ya ufadhili wa Tanapa.
Mbunge huyo, alisema kuwa kumekuwa na matukio mengi ya  ujangili katika maeneo mengi sasa hivi kutokana na baadhi ya  watu kujihusisha na biashara haramu ya pembe za ndovu na nyama  pori.
Aidha, alisema kuwa kijana wa kitanzania kujihusisha na vitendo vya ujangili ni kukosa uzalendo ndani ya nchi yao kwa kushiriki  kufanya uhujumu.
Hata hivyo, alisema kama mbunge yupo tayari kusaidia vikundi  vya vijana mitaji ili waweze kuacha kujiingiza katika matukio ya  ujangili.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa