Home » » ULANGA WACHACHAMAA

ULANGA WACHACHAMAA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WANANCHI wa Tarafa ya Malinyi Wilayani ya Ulanga mkoani Morogoro, wametaka kufahamu hatua zilizochukuliwa na Serikali baada ya mauaji ya kupigwa risasi kwa raia yanayodaiwa kufanywa na askari watatu wa eneo hilo.
Mauaji hayo yalifanyika wakati wa maandamano ya amani kupinga unyanyasaji, ucheleweshaji wa kesi na uonevu uliokuwa ukifanywa kwao na baadhi ya askari wa kituo hicho.
Kilio hicho kilitolewa katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Malinyi ambapo mmoja wao, Protas Itema alisema wanashangazwa kuona serikali iko kimya hadi sasa kufuatia mauaji hayo.
Mbunge wa Ulanga Magharibi, Dk. Juma Mponda aliwataka wananchi hao kuwa watulivu kwa vile aerikali imeshaanza kuchukua hatua ikiwemo kufanya mabadiliko ya askari wa kituo cha polisi Malinyi.
Alisema  kazi ya polisi ni kulinda raia na mali zao lakini hawataweza kufanikiwa bila wananchi kuwapa ushirikiano ili kuwatia mbaroni watuhumiwa wanaohusika na vitendo mbalimbali vya kiuhalifu, yakiwemo mauaji ya mfululizo yaliyojitokeza.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa