Home » » MISS KANDA MASHARIKI VIPAJI IDD PILI

MISS KANDA MASHARIKI VIPAJI IDD PILI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Warembo 14 wanaowania taji la Kanda ya Mashariki (Redd’s Miss Eastern Zone 2014) watashindania taji la vipaji (Talent Award), lililopangwa kufanyika siku ya Idd Pili kwenye Ukumbi wa Maisha Plus, Kibaha, Pwani.
Mratibu wa mashindano hayo, Alex Nikitas alisema kutokana na mashindano hayo ya vipaji, kambi ya warembo iliyopangwa kuanza Julai 29 kwenye hotel ya Usambara Safari Lodge, sasa itaanza Julai 28 kwenye hotel ya Precision mkoani Pwani.
Nikitas alisema maandalizi ya mashindano hayo yamekamilika na warembo hao, mbali ya kushindana katika vipaji, pia watatoa msaada kwa kituo cha watoto yatima cha Mkoa wa Pwani na baadaye kurejea mkoani Morogoro tayari kwa mashindano yaliyopangwa kufanyika Nashera Hotel Agosti 8.
“Maandalizi yanaendelea vizuri ambapo tunategemea taji hili msimu huu litakwenda kwa mrembo mwenye vigezo atakayeiwakilisha kanda yetu vema katika fainali za taifa baadaye mwaka huu,” alisema Nikitas.
Alisema mashindano hayo yatashirikisha jumla ya warembo 14 kutoka mikoa minne, ambayo ni Pwani, Lindi, Mtwara na wenyeji Morogoro.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa