Home » » MAKALLA AMWAGA VIFAA JIMBONI

MAKALLA AMWAGA VIFAA JIMBONI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
TIMU 23 za soka kutoka kata za Wilaya ya Mvomero, Mkoa wa Morogoro zimepatiwa vifaa vya michezo kuelekea michuano ya kuibua vipaji ambapo mechi zake zitakuwa zikifuatiliwa kwa karibu na makocha wa timu za Yanga, Azam, Simba na Mtibwa Sugar.
Michuano hiyo inayofahamika kama Makalla Cup, itaanzia ngazi ya kata ikishirikisha timu za vijiji vyote kisha kuchezwa ngazi ya tarafa na wilaya huku makocha wa timu hizo kubwa wakiangalia vijana wenye vibaji.
Naibu Waziri wa Wizara ya Maji, Amos Makalla, ambaye ni mbunge wa Mvomero, akitoa vifaa hivyo, alisema michuano hiyo itaanza leo kwa mfumo wa mtoano huku zawadi ikiwa ni kwa timu ya kwanza na pili.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Dakawa wakati wa kugawa jezi na mipira kwa kila kata,  Makalla alisema michuano hiyo imeboreshwa zaidi ikiewemo waamuzi kutoka nje ya wilaya hiyo.
“Kila hatua  ya mashindano ngazi ya kata washindi wa kwanza hadi wa tatu watapata zawadi, ni pamoja na ngazi ya tarafa  hadi wilaya na zawadi nono zaidi inayofiki sh milioni moja atapewa bingwa wa wilaya ” alisema Makalla  baada ya kugawa vifaa.
Mbali ya kuanika zawadi, alisema katika hatua ya timu nane bora, atawaleta makocha wasaidizi wa timu za Simba, Yanga, Azam na Mtibwa Sugar kuangalia vipaji.
Licha ya kutoa mipira kwa ajili ya mashindano hayo, pia alizikabidhi mipira na jezi timu za soka za vijiji, shule za msingi na sekondari katika vijiji vya Dakawa,   Mlali, Kipera, Mkindo, Kibogoji, Lungo, Dihinda,  Pemba na timu za netiboli ili   kuendeleza na kuinua michezo vijijini.
Baadhi ya timu za soka za Dakawa zilizokabidhiwa jezi na mipira, ni Small Boys, Young Boys, Veteran FC, Juvinali FC  na Dakawa Rangers.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, viongozi wa timu hizo walimpongeza Makalla kwa kujali maendeleo ya soka na vijana kwa ujumla.
Mbunge huyo ameahidi kuvisaidia pia vikundi vya sanaa vilivyoanzishwa vijijini vikiwemo vya kareti vya vijiji vya Dihinda na Dakawa
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa