Home » » VIONGOZI WAVAKIA NJUGA VIMEMO

VIONGOZI WAVAKIA NJUGA VIMEMO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

VIONGOZI wa serikali za vijiji vya Kata ya Maguha na Magubike, mkoani Morogoro, wameazimia kusambaratisha na kukomesha migogoro ya ardhi kwa kuvifikisha mahakamani vikaratasi vyote vya kugawana ardhi kwa njia ya panya.
Maazimio hayo yaliyofikiwa mwishoni mwa wiki kwenye mafunzo ya sera na sheria za ardhi nchini yaliyoandaliwa na asasi ya Dira na Foundation for Civil Society – FCS, yalikwenda sambamba na mchakato wa kutunga sheria ndogondogo katika vijiji hivyo kuwadhibiti viongozi watakaokiuka.
Sambamba na maazimio hayo, pia wamekubaliana hadi kufikia Agosti mwaka huu, vijiji viainishe na kutafuta suluhu ya migogoro ya ardhi katika vijiji husika, viwe na masijala na wananchi wapatiwe hati za kimila kumiliki ardhi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, viongozi hao wakiongozwa na Diwani wa Magubike, Ernest Chilolo na Mtendaji Kata, James Mnghondwa, walisema wamechoshwa na migogoro isiyoisha na kurudisha nyuma maendeleo ya wananchi.
“Cha msingi hakuna haja kukaa tukiwalea wanaotuangamiza, ni bora tukaonekana wabaya kwa kuzuia ardhi yetu isiporwe na wachache kwa faida zao na kutuacha tukiumia,” alisema Diwani Chilolo.
Akihitimisha mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Dira, Erasmo Tulo, alisema tayari asasi hiyo imeendesha mafunzo kwa sanaa vijijini humo na kubaini changamoto mbalimbali ikiwemo ya wananchi kutozielewa sera na sheria za ardhi na kusababisha migogoro isiyoisha.
“Hii ni awamu ya pili ya mafunzo haya, tunachotegemea kwenu kwanza ni migogoro ipungue kwa zaidi ya asilimia 90 na wananchi watendeeni haki kwa kuwamilikisha ardhi, ili kila mmoja awe na nguvu ya umiki,” alisema.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa