Home » » ALAT YAWAKUMBUSHA MADIWANI WAJIBU WAO

ALAT YAWAKUMBUSHA MADIWANI WAJIBU WAO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
KATIBU Mkuu wa Jumuiya ya Serikali za Mitaa Tanzania (ALAT), Abraham Shamumoyo, amewataka madiwani kusimamia fedha za miradi ya maendeleo zinazopelekwa na serikali kwenye halmashauri zao.
Shamumoyo alisema hayo jana wakati akikagua miradi ya maendeleo kwenye  maadhimisho ya Wiki ya Serikali za Mitaa mkoani hapa, inayotekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Muheza.
Alisema kuna baadhi ya halmashauri zimeshindwa kusimamia miradi ya maendeleo kwa ufanisi badala yake zimekuwa zikitumia fedha nyingi kwenye miradi ambayo hailingani na thamani halisi ya fedha zilizotumika.
“Kuna baadhi za halmashauri humu nchini ukienda unakuta miradi iliyotekelezwa ipo chini ya viwango, hadi ukuta unataka kuanguka kutokana na kujengwa chini ya kiwango,” alisema Shamumoyo.
Pia alishauri halmashauri kutekeleza miradi yake kwa ubora ili kuongeza fedha pindi wanapotaka kuomba fedha za kuendesha miradi mingine.
Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, Gulamhafeez Mukadam, alisema tatizo la makandarasi wengi kujenga miradi chini ya viwango limekuwa likisumbua halmashauri nyingi nchini.
“Kwa mfano kwetu Shinyanga, mradi mmoja umekuwa ukitekelezwa na zaidi ya wakandarasi watatu hadi wanne kutokana na kila ukikagua unakutana na upungufu, hali hii inachelewesha miradi mingi kukamilika kwa wakati,” alisema Meya Mukadam.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, Amir Kiroboto, alisema siri ya mafaniko ya miradi yao kuwa bora inatokana na usimamizi mzuri kuanzia kwa madiwani hadi kwa wataalamu wa halmashauri hiyo.
Chanzo:Tanznia Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa