Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Akizungumzia hilo mjini hapa jana, Mkuu wa Wilaya ya Kilombero,
Hassan Masala, alisema kati ya miradi hiyo mmoja ni maabara ya Shule ya
Sekondari Mlabani, Ifakara.
“Miradi miwili ukiwemo wa nyumba ya mganga Sagamaganga na mashine ya
kusaga na kukoboa Mang’ula A, imezinduliwa na miradi mitatu ukiwemo wa
barabara ya lami ya Uhuru Ifakara, mradi wa maji Signal na Ofisi ya
Kijiji Mang’ula A imewekwa jiwe la msingi,” alifafanua Masala.
Kwa mujibu wa Masala, mwenge huo ulikagua na kujionea miradi ya
vikundi vya wanawake, wanaume, vijana, mradi wa ufugaji nyuki na hifadhi
ya mazingira na shughuli za kupambana na kuzuia rushwa.
“Kati ya fedha hizo, sh milioni 136.9 zimechangwa na wananchi, sh
milioni 463.8 serikali kuu, sh milioni 5.8 halmashauri na wahisani sh
milioni 422.9,” alisema.
Chanzo:Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment