Home » » WATOTO ASILIMIA 62 MORO WAFANYIWA UKATILI

WATOTO ASILIMIA 62 MORO WAFANYIWA UKATILI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
TAASISI ya Tanzania Women Health Network (TWHN), imebaini kuwa zaidi ya asilimia 62 ya watoto katika Manispaa ya Morogoro, wamefanyiwa ukatili wa kisaikolojia, jinsia na kimwili na watu wa karibu, wakiwemo ndugu na jamaa.
Hayo yamo kwenye taarifa fupi ya uzinduzi wa taasisi hiyo iliyosomwa na Mkurugenzi wake, Gloria Kasilo kwa Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Said Amanzi, aliyewakilishwa na Ofisa Elimu Taaluma wa manispaa hiyo, Christopher Wangwe.
“Ukatili mkubwa uliobainika katika utafiti huu hususani shule moja ya msingi iliyotumika kama sampo ni ngono, kutumika kutafuata riziki, kupigwa, kutumikishwa majumbani na kutishwa na wengine kufichwa,” alisema.
Alisema lengo la taasisi hiyo ni kumwezesha mwanamke hasa mtoto wa kike kujikomboa kwa kupata elimu itakayomwezesha kuzikabili changamoto katika mazingira walipo na hatimaye kujiletea maendeleo.
Wangwe mbali na kuahidi kuunga mkono taasisi hiyo ili kufikia mpango wa serikali wa Matokeo Makubwa  Sasa, aliziomba taasisi na asasi zote za kiraia kusaidia kudhibiti vitendo hivyo pamoja na wimbi la matumizi ya dawa za kulevya.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa