Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
CHUO Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimeanza kampeni ya
nguvukazi kupanda miti kuzunguka Bwawa la Mindu linalotegemewa kwa
zaidi ya asilimia 70 katika kutoa huduma ya maji safi na salama ili
kutokausha maji hususan nyakati za kiangazi.
Kampeni hiyo ilizinduliwa mjini hapa juzi na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Said Amanzi.
Akizindua kampeni hiyo, Amanzi mbali na kukipongeza chuo kubuni
mpango huo alisema kutokana na uharibifu wa mazingira uliopo nchini
nchi inakabiliwa na changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi katika
baadhi ya maeneo.
Makamu Mkuu wa SUA, Profesa Gerald Monela, alisema licha ya chuo
hicho kuwa na mafanikio bado kinakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo
ya baadhi ya wananchi kuvamia eneo la chuo.
Alisema licha ya chuo kushirikisha jamii kutunza mazingira, jamii
imekuwa ikikiuka taratibu na kuendeleza kukata miti hovyo, uchomaji wa
misitu na kufanya shughuli nyingine katika maeneo hayo.
Naye Mkuu wa Kitivo cha Misitu na Hifadhi ya Mazingira, Yonika Ngaga,
alisema lengo la kuadhimisha siku ya upandaji miti ni kuipa hamasa
jamii kutunza mazingira, pamoja na kulinda mipaka ya chuo isiharibiwe
pamoja na mipaka ya Bwawa la Mindu.
Uzinduzi wa upandaji miti unafanyika kila Aprili mosi, lengo likiwa ni kuhamasisha jamii juu ya utunzaji wa mazingira.
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment