Home » » Shirika lapinga matumizi ya vidhibiti mimba

Shirika lapinga matumizi ya vidhibiti mimba

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MAKOVU ya kudumu  kwa wanawake wengi nchini husababishwa na  utoaji mimba pamoja na utumiaji wa vidhibiti mimba ambayo ni hatari kwa afya zao.
Kauli hiyo ilitolewa mjini hapa juzi na Mkurugenzi wa Shirika la Kutetea Uhai (Prolife), Emil Hagamu, kwenye mafunzo juu ya utumiaji wa vidhibiti mimba kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Jodani na Chuo cha Uandishi wa Habari cha Morogoro (MSJ).
Hagamu alisema vidhibiti vina madhara makubwa kwa watumiaji ambavyo vinaweza kuhatarisha maisha na kusababisha kifo.
“Kuna madhara mengi yakiwemo kuharibika ubongo, moyo kwenda mbio, kuharibika mapafu, kuumwa chini ya kitovu na kupata saratani ya tumbo la uzazi. Pia husababisha mzunguko wa hedhi kubadilika na mara nyingine husababisha kutokuzaa kabisa,” alisema.
Aliwataka wana vyuo hao kutumia njia za asili kuzuia mimba na kuepuka matumizi ya vidhibiti mimba.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa