Home » » SHAMBA LA SUMAYE MVOMERO CHANZO UHARIBIFU MAZINGIRA

SHAMBA LA SUMAYE MVOMERO CHANZO UHARIBIFU MAZINGIRA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
SHAMBA la Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya tatu, Fredrick Sumaye, lililopo Kijiji cha Mvomero wilayani hapa, limetajwa kuwa chanzo cha uhaba wa ardhi na uharibifu wa mazingira kutokana na kuwalazimisha wananchi kukimbilia kwenye maeneo tengefu ya kutunza mazingiria milimani.
Sambamba na madai hayo, Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero imetajwa kuchochea uharibifu wa mazingira kwa kukalia sheria ndogondogo walizotunga wananchi kwa lengo la kupambana na waharibifu wa mazingira, wakiwemo wavamizi.
Hayo yalibainishwa juzi kwenye mdahalo wa wananchi na viongozi ulioitishwa na asasi ya mazingira mkoani Morogoro (Conasu) na Mtandao wa Mazingira Tanzania (Manet) kwa hisani ya Mfuko wa Hifadhi ya Wanyamapori Duniani (WWF) kujadili njia ya kuhifadhi pamoja msitu.
Akiongoza mdahalo huo, mwezeshaji kutoka Conasu, Ahmed Mdangu, aliwataka washiriki kuainisha changamoto zinazosababisha milima tegemeo kwa vyanzo vya maji na hewa safi kuharibika.
“Fursa pekee waliyonayo Watanzania ni ardhi inayowazunguka… kuna changamoto nyingi zinazotukabili ikiwemo iliyo usoni ya Jumuia ya Afrika Mashariki, kwa hiyo wananchi tuamke na kulinda maeneo yetu kwa faida ya kizazi cha leo na kijacho,” alisema Mdangu.
Kutokana agizo hilo, washiriki wakiwemo Hamadi Binsaki, Paulina Anthon na Mohamed Lundenga, walisema wamewahi kutunga sheria ndogo ya kulinda mazingira, lakini halmashauri imezikalia na hakuna kiongozi anayetaka kuzizungumzia.
Binsaki alisema uharibifu mkubwa umeibuka miaka ya karibuni kutokana na eneo kubwa la kijiji hicho kupewa mwekezaji waliyemtaja kuwa Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya tatu, Sumaye.
Alisema kupewa kwa eneo hilo kwa mwekezaji huyo pia kuliibua hofu kubwa ya usalama kwa wanakijiji baada ya baadhi walioonekana kuwa msitari wa mbele kudai uhalali huo kukamatwa na kuwekwa ndani.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa