Home » » WANANCHI WATAKIWA KUJITOKEZA KUCHANGIA DAMU

WANANCHI WATAKIWA KUJITOKEZA KUCHANGIA DAMU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WANANCHI wa Mkoa wa Morogoro wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuchangia damu kwa hiari katika maadhimisho ya Wiki ya Damu, ikiwa ni utekelezaji wa mpango wa taifa wa damu salama.
Wito huo ulitolewa na Ofisa uhamasishaji elimu kwa umma, Wille Mathew, katika kituo kidogo cha  uchangiaji damu na kusema kuwa zoezi hilo linatarajiwa kuanza rasmi Machi 18, mwaka huu  na kudumu kwa muda wa wiki moja.
Alisema zoezi hilo litashirikisha vyuo vilivyopo mkoani humo kikiwemo chuo cha ujenzi, Jordan University, chuo cha mifugo, Chuo cha Uislamu, Saint Joseph pamoja na taasisi nyingine za elimu zikiwemo Lutheran Junior Seminary  na Shule ya Sekondari  Presybeterian.
Chanzo:Tanzania daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa