Home » » Polisi Morogoro yarudi Ligi Kuu Bara

Polisi Morogoro yarudi Ligi Kuu Bara

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Bao lililofungwa na James Mganda dakika ya 26 lilitosha kuiwezesha Polisi Morogoro kurejea Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Maji Maji ya Songea katika mchezo wa ligi daraja la kwanza uliochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri Morogoro.
Polisi Moro inayonolewa na kocha Richard Adolph ilikuwa ikihitaji ushindi wa namna yoyote katika mechi hiyo, ambapo dakika ya sita nahodha wake Nahoda Bakari alimimina krosi iliyomkutana na Mfuko Abdallah ambaye aliukwamisha mpira nyavuni.
Bao hilo liliwachanganya Majimaji na kusababisha mambo yawaendee kombo kwani dakika ya 26 waliruhusu kufungwa bao la pili na, James Mganda anayechezea timu ya taifa ya vijana (Serengeti Boys U17).
Mganda alifunga bao hilo baada ya kutumia vema pasi nzuri ya Nicolaus Kabipe.
Kipindi cha pili Majimaji inayonolewa na kocha Hassan Banyai ilikianza kwa nguvu, ambapo ilipata bao la kufutia machozi dakika ya 79 lililofungwa na Anthony Mwingira.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa