Home » » Uandikishaji walemavu shule waongezeka

Uandikishaji walemavu shule waongezeka

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
UANDIKISHAJI wa watoto wenye ulemavu katika shule za msingi wilayani Kilombero umeongezeka kutoka watoto 131 mwaka 2012 hadi watoto 160 mwaka jana.
Hayo yamo kwenye taarifa ya utafiti wa pili juu ya vikwazo wanavyopata wenye ulemavu katika kupata elimu uliofanywa na vyama vitano vya wenye ulemavu wilayani Kilombero kupitia mradi wa kuboresha uelewa na utetezi kwa jamii (ICAAD) na taasisi ya Kesho Trust Tanzania kwa kufadhiliwa na shirika la misaada ya kimaendeleo nchini Uingereza (UK Aid).
Mratibu wa mradi wa ICAAD Kilombero, Lucas Liombechi, alisema vyama vilivyoshiriki katika utafiti huo Kata ya Ifakara, Kibaoni na Lumemo ni Chama cha Wasioona (TLB), Chama cha Viziwi Tanzania (CHAVITA), Chama cha Walemavu Tanzania (Chawata), Chama cha Albino Tanzania (TAS) na Chama cha Wenye Ulemavu Tanzania (TAMH).
Chanzo;Tanzania  Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa