Home » » Wananchi watakiwa kufuatilia

Wananchi watakiwa kufuatilia

Kukosekana kwa elimu ya ufuatiliaji fedha za umma kwa wananchi wengi, kumesababisha ongezeko la utekelezaji miradi ya maendeleo hususan maeneo ya vijijini kufanywa chini ya kiwango.
Baadhi ya wananchi wa Mji Mdogo wa Kimamba, wilayani Kilosa; Ramadhan Liwest, Aishi Ally na Yahya Mhina walisema hayo walipozungumza na waandishi wa habari.
Walishauri ni vyema jamii ikapewa mafunzo ya kuwajengea ufahamu wa kuhoji mapato na matumizi, hasa idara zinazogusa moja kwa moja jamii; Elimu na afya.
Kauli ya wananchi hao imekuja huku tayari asasi isiyokuwa ya Serikali ya Kilosa African Youth Organization (Kayo), ikiwa imeanza kuwezesha wananchi hao kuhusu mbinu za Ufuatiliaji Matumizi ya Rasilimali za Umma (Pets) kwenye idara ya afya.
Mratibu wa Kayo, Ramadhan Nassoro na Katibu wake, Juma Mseti kwa nyakati tofauti walisema wameamua kutoa mafunzo hayo ili wananchi wajitambue na kufahamu wajibu wao kufuatilia fedha na rasilimali za umma.
Nassoro alisema wananchi wanaweza kufanya jukumu hilo kama vikundi kwa kufuatilia matumizi na mapato, ikiwamo vituo vya afya na zahanati na kwamba kufanya hivyo kutasaidia ufanisi wa utekelezaji majukumu mbalimbali.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa