Home » » Wanawake wamjia juu DC wa Mvomero

Wanawake wamjia juu DC wa Mvomero

Morogoro. Jumuiya wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) ya Chama cha Mapinduzi(CCM) Wilaya ya Mvomero, imelaani vikali kauli zilizotolewa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Antony Mtaka kwa kuwafananisha wanawake na ‘kondomu’ ama tambara la deki.
Baadhi ya wanawake ambao ni Wajumbe wa Baraza la UWT Mvomero ambao hawakutaka majina yao kuandikwa gazetini walisema mkuu huyo wa wilaya aliwataka wanawake kutokutumiwa vibaya wakati wa chaguzi zijazo kauli ambayo wanawake hao hawakupendezwa nayo.
Wakizungumza na waandishi wa habari mjini Morogoro wanawake hao walisema baada ya kufanyika kwa baraza Desemba 12 mwaka huu katika ofisi za CCM Dakawa wilayani Mvomero ambapo DC Mtaka alikuwa mgeni rasmi, wamekaa na kutafakari kauli hiyo na kuona kuwa ni ya udhalilishaji kwa wanawake kufananishwa na kondomu au tambara la deki
Walidai kuwa mkuu huyo wa wilaya alialikwa kwenye baraza hilo na baada ya kupewa nafasi ya kuzungumza na wajumbe aliwaambia wasikubali kutumika kama kondomu ama tambara la deki na wanasiasa wanaowania nafasi mbalimbali wakati wa uchaguzi ujao.
“Kauli alizotoa Mtaka si nzuri zimetusikitisha sana, anatuambia sisi kinamama ni kama kondomu ambayo ikishatumika inatupwa, ama tambara la deki ukidekia halina thamani tena, kauli hii si ya kiungwana walisema.
Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Antony Mtaka akijibu tuhuma hizo, alikiri kutumia kauli hizo na kwamba hakuwa na nia mbaya kama wao walivyofikiria isipokuwa hizo ni siasa chafu za baadhi ya wanasiaa wa Mvomero .
Mtaka alisema Jumuiya hiyo ni kubwa ndani ya CCM na kwamba kuna viongozi wengi wa siasa lakini cha kushangaza hakuna hata mmoja aliyeichangia jumuiya hiyo ili iweze kufanikiwa.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa