Home » » Maofisa Moro watembelea daraja la Mwere

Maofisa Moro watembelea daraja la Mwere

Daraja la MwereHATIMAYE Halmashauri ya Manispaa Morogoro kupitia mhandisi wake wa ujenzi, Eriki Ntambi, imetoa ufafanuzi juu ya kupasuka kwa daraja jipya la Mwere lililojengwa kwa zaidi ya sh bilioni 1.6.
Akiwa ameongozana na jopo la wataalamu sambamba na Meya wa Manispaa hiyo, Amir Nondo, Ntambi alisema ufa ulioripotiwa na unaoonekana katika daraja hilo ni zege maalumu iliyowekwa kuondoshea maji ya mvua kwa urahisi.
“Mpasuko huu sio wa daraja ni zege iliyowekwa juu kuinua mgongo, ili kuondoshea maji ya mvua kwa urahisi…na hili tunaweza kulikwangua tukaliondoa lote bila kuathiri daraja hili,” alisema Ntambi.
Meya Nondo alisema daraja hilo limejengwa kwa kuzingatia aina zote za vipimo na ni daraja pekee la mfano mjini humo maalumu kupunguzia msongamano wa vyombo vya moto kati kati ya mji huo.
“Unajua daraja hili lilivyojengwa limepachikwa hapa juu hata kama itatokea kupata dhoruba yoyote ni rahisi kuondolewa na kupachikwa jingine…huu ni mfumo wa kisasa wa kitaalamu katika ujenzi madaraja; wananchi wawe huru kulitumia,” alisisitiza Nondo.
Hivi karibuni Tanzania Daima ilitoa taarifa ikionyesha hofu ya daraja hilo kukatika ikiwa ni miezi michache tangu kukabidhiwa.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa