Kiwanda hicho ambacho awali kilimilikiwa na serikali kabla ya
kubinafsishwa mwaka 1998 kilifahamika kwa jina la Morogoro Polyster
Textile Limited .
Akifungua mafunzo ya wataalamu wa kuandaa programu ya wizara hiyo
waliokutana mjini hapa, Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Magembe,
aliitaka ofisi ya mkoa kukifunga kiwanda hicho hadi kitakaporekebisha
miundombinu yake.
Profesa Maghembe alisema wakati taifa linahangaika kusogeza huduma ya
majisafi na salama jirani na makazi ya watu nchini, haitaweza
kuwavumilia na kuwakumbatia wawekezaji wanaohatarisha maisha ya
viumbehai.
“Ni kweli serikali inahitaji wawekezaji, lakini sio wanaokiuka
mikataba na masharti ya utunzaji wa mazingira…tutafunga viwanda vyote
vinavyosababisha uharibifu wa mazingira,” alisema Profesa Magembe.
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment