Home » » RC Moro ashauri benki kufikisha huduma vijijini

RC Moro ashauri benki kufikisha huduma vijijini

MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera, amezishauri benki kuweka vipaumbele katika kutoa huduma za kibenki kwa wafanyabiashara wadogo na wajasiriamali kwa kufungua matawi mengi ya huduma hizo vijijini.
Mkuu wa Mkoa alitoa changamoto hiyo hivi karibuni wakati wa hafla ya ufunguzi wa Tawi la 18 la Benki ya Diamond Trust Tanzania (DTB) lililopo mkoani hapa.
Alisema, huduma za kibenki zinahitajika zaidi maeneo ya vijijini ambako wananchi wengi ni wazalishaji mali na waendeshaji wa biashara ndogo ili waweze kuhifadhi fedha zao kwa usalama.
Naye Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo, Viju Cherian , alisema ufunguzi wa tawi hilo katika Mkoa wa Morogoro ni uthibitisho wa mafanikio ya lengo la benki kupanuka kijiografia nchini Tanzania kwa kuwafikia wateja Watanzania waliowengi katika sehemu za vijijini.
Kwa mjibu wa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki hiyo, DTB ina matawi katika Jiji la Dar es Salaam, Arusha , Mwanza , Zanzibar, Dodoma , Tanga , Mbeya ,Kilimanjaro, Iringa na sasa Morogoro.
Benki hiyo yenye makao yake makuu jijini Nairobi, ina jumla ya matawi 95 katika nchi nne za Afrika Mashariki , ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda na Burundi.
Chanzo;Habari Leo

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa