Home » » Mlinzi auawa lindoni Moro

Mlinzi auawa lindoni Moro

Morogoro. Watu watatu wamefariki dunia katika matukio tofauti yaliyotokea mkoani Morogoro likiwemo la mlinzi wa mnara wa kampuni ya simu kuuawa kwa kupigwa na kitu chenye ncha kali kichwani wakati akiwa lindoni.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Faustine Shilogile alimtaja mlinzi aliyeuawa kuwa ni Hamisi Mtini (65) Mkazi wa Kihonda Mbuyuni Manispaa ya Morogoro.
Alisema tukio hilo lilitokea Desemba 29 mwaka huu saa 1:30 asubuhi eneo la Kihonda Mbuyuni ambapo mlinzi huyo aliuawa na watu wasiojulikana kisha watu hao waliiba betri za mnara wa Kampuni ya Simu ya Tigo.
Aidha Mwanne Omary (43) Mkazi wa Ipugusa Mlimba Wilaya ya Kilombero ameuawa kwa kukatwa mapanga shingoni na ubavuni na watu wasiofahamika huku chanzo kikidaiwa kuwa ni imani za kishirikina.
Shilogile alisema tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Desemba 27 mwaka huu katika Tarafa ya Mlimba Wilaya ya Kilombero.
Huko maeneo ya mashamba ya Agrofocus Kata ya Magomeni Wilaya ya Kilosa, mtu ambaye hakufahamika amekutwa amekufa na mwili wake ukining’inia kwenye mti baada ya kujinyonga.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa