Kilosa. Migogoro ya ardhi wilayani Kilosa,
Morogoro, itaikosesha mapato halmashauri ya wilaya hiyo, baada ya
wafugaji kuazimia kutouza mifugo yao kwenye mnada mkubwa wa mifugo wa
Dumila na badala yake kuhamishia shughuli hizo huko Mikongeni katika
Barabara ya Morogoro-Dodoma, wilayani Mvomero.
Hayo yalibainishwa juzi katika mjadala wa mafunzo
kwa viongozi wa serikali, dini taasisi na wanachi, yaliyoandaliwa kwa
ushirikiano wa Greenbelt School Trust Fund (GSTF) The Foundation for
Civil Society.
Wakizungumza kwenye mjadala huo, Ibrahim Poromoka
wa Kitete na Michael Kashu wa Ngoisani- Mabwegere, walielezea wasiwasi
wao kuhusu kuporomoka mara dufu, mapato ya Halamashauri ya Kilosa kama
hakutakuwa na hatua madhubuti za kulikabili tatizo hilo.
“Migogoro ya ardhi ni mingi ukiwamo wa wakulima na
wafugaji, mipaka baina ya vijiji na vijiji na ile ya mtu na mtu lakini
kubwa hapa ni wenzetu wafugaji kuikosesha mapato Serikali ya wilaya
Kilosa kwa kuua Mnada wa Dumila na kwenda kuendeleza Mnada wa Mkongeni
wilayani Mvomero,” alisema Poromoka.
Alisema bila kujali kuwa mnada huo una manufaa
makubwa kwao na Serikali ya wilaya hiyo. Wafugaji hao jamii ya Kimasai,
wameamua kutouzia mifugo yao kwenye mnada huo wa Dumila.
Kashu ambaye ni mfugaji wa jamii ya Kimasai,
alisema uamuzi wa kuhamishia shughuli zao katika mnada wa Mkongeni,
umefanywa na mikutano ya mila na makundi mbalimbali ya jamii hiyo
wakiwamo Morani.
“Hakuna mtu anayependa ugomvi, kisa cha wafugaji
kuhama Mnada wa Dumila na kwenda Mkongeni ni vurugu zilitokea Machi
mwaka huu na kusababisha barabara kuu kufungwa,” alisema Kashu.
Alisema baada ya tukio hilo, makundi ya kimila ya
Wamasai yalikutana na kujadili hali iliyojitokeza na hatimaye kuhamisha
Mnada wa Dumila.
Hata hivyo Katibu wa GSTF John Mengele na ofisa
tarafa hiyo ya Magole Moses Nchimbi waliwataka viongozi wa serikali za
vijiji na kata kufanya kazi ya ziada kutatua migogoro mapema.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment