Home » » Vikundi vya ujasiriamali

Vikundi vya ujasiriamali

Morogoro.Vijana mkoani hapa wametakiwa kujiunga na vikundi vya ujasiriamali kuliko kuwa tegemezi katika jamii na wengine kujiingiza katika makundi maovu ya matumizi ya dawa za kulevya.
Hayo yalisemwa hivi karibuni na Diwani wa Kata ya Kingo, Fidelis Tairo alipokuwa akizungumza na gazeti hili..
Tairo alisema jamii ya sasa imekuwa na vijana wengi ambao hawapendi kujishughulisha katika uzalishaji , hivyo kujikuta wakishindwa kuchangia pato la Taifa.
Alisema ni bora vijana wakajiunga katika vikundi mbalimbali vya Kuweka na Kukopa (Saccos) ili kuweza kuchukua fedha za mkopo kwa lengo la kuzitumia katika uendeshaji wa biashara ndogondogo.
“Vijana mnatakiwa kujiunga katika vikundi vya kuweka na kukopa kuliko kuwa tegemezi katika jamii kwakuwa nyinyi mnategemewa katika uzalishaji na kuongeza pato la taifa, msitumie nguvu zenu katika kufanya maovu na kuishia jela”alisema 

chanzo;mwananchi.

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa