Home » » Mwanasheria ataja chanzo migogoro mabaraza ya ardhi

Mwanasheria ataja chanzo migogoro mabaraza ya ardhi


na Ghisa Abby, Morogoro

MWANASHERIA na mtetezi wa haki za binadamu Mkoa wa Morogoro, Amani Mwaipaja, amesema kutokuwapo kwa usimamizi mzuri katika mabaraza ya ardhi ya kata kunasababisha kutokea kwa migogoro kati ya kijiji na kijiji.
Mwaipaja alisema hayo jana alipozungumza na Tanzania Daima ofisini kwake juu ya migogoro ya ardhi ya mara kwa mara.
Alisema migogoro hiyo pia inasababishwa na baadhi ya watendaji wa vijiji na kata wasiowajibika ipasavyo kwa wananchi.
“Mara nyingi usimimizi mbovu wa ardhi kuanzia ngazi ya chini ndio chanzo kikuu cha kuibuka kwa migogoro kati ya wakulima na wafugaji katika Mkoa wa Morogoro na maeneo mengine,” alisema Mwaipaja.
Aidha, alisema ili kuhakikisha changamoto hiyo inapatiwa ufumbuzi wa kudumu ni vema serikali ikaweka mfumo maalumu wa kutoa elimu kwa wananchi juu ya usimamizi na matumizi bora ya ardhi.
Pia aliwaasa wananchi kuepuka kuuziwa ardhi kiholela bila ya kupatiwa kibali maalumu kutoka kwa maofisa wa ardhi, kwani kushindwa kufanya hivyo kutachangia kukosa hatimiliki


CHANZO TANZANIA DAIMA GAZETI

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa