Home » » NDALICHAKO: FEDHA ZA SERIKALI SI ZA KUGAWANA POSHO

NDALICHAKO: FEDHA ZA SERIKALI SI ZA KUGAWANA POSHO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Imeandikwa na John Nditi, Morogoro
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako
WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako amewataka viongozi wa taasisi mbalimbali katika wizara hiyo, kutumia fedha kulingana na miongozo ya serikali na si kugawana kwa kulipana posho za nyumba, vikao na safari za nje kinyume na taratibu na maelekezo ya serikali.
Profesa Ndalichako alisema hayo juzi mjini Morogoro, wakati akifungua mkutano wa viongozi wa taasisi zilizo chini ya wizara hiyo, ambao umelenga kuchanganua viashiria hatarishi katika sekta ya elimu na namna ya kuboresha utekelezaji wa mifumo ya viashiria hivyo katika maeneo yao ya kazi ili kukuza na kuendeleza elimu nchini.
Waziri huyo alisema kuwa; “Baadhi ya changamoto zinazoikumba taasisi zilizopo chini ya wizara yangu ni ukosefu wa maadili, upungufu wa wataalamu, vifaa, miundombinu zinazosababishwa na baadhi ya viongozi kutumia fedha kinyume na utaratibu.”
Alisema kwa muda mrefu kumekuwa na tabia kwa baadhi ya viongozi wa taasisi za wizara hiyo, kuona kuwa taasisi hizo haziko chini ya serikali na kutofuata miongozo ya utumishi wa umma. Alisema wizara haina chanzo chochote cha kuingiza mapato, hivyo ni wajibu kwa viongozi wa taasisi mbalimbali katika sekta ziliz ochini ya wizara kutumia fedha kulingana na miongozo ya serikali na si kugawana kiholela.
“Si vizuri kuendelea kujilimbikizia fedha za serikali, na ni vizuri kutumia fedha hizo kulipa malimbikizo na madeni ya wafanyakazi pamoja na kuwannulia vitendea kazi,” alisema Profesa Ndalichako.
Kutokana na hali hiyo, alimwagiza Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk Leonard Akwilapo kuandika mwongozo wa serikali ili watakaoukiuka matumizi ya fedha za umma washughulikiwe kwa mujibu wa sheria.
Pamoja na hayo, aliwataka viongozi hao kuacha kuwasubiri viongozi wa juu kufuatilia mikataba wanayoingia na wadau wengine badala yake wawe wa kwanza wao kufuatilia miradi hiyo na kuisimamia Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, kwa nyakati tofauti, waliahidi kutumia mafunzo hayo na kutekeleza maagizo ya waziri kwa lengo la kuleta ufanisi.
CHANZO HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa