MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Dk Stepen Kebwe amemtaka mkandarasi ambaye
ni Wakala wa Majengo wa Serikali (TBA) kuongeza kasi ya ukarabati wa
jengo la kuhifadhia maiti (mochwari) katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa
wa Morogoro ili ukamilike ndani ya wiki mbili zijazo.
Alisema hayo juzi alipofanya ziara kukagua maendeleo ya ukarabati huo
baada ya kumalizika kwa zoezi la usafi wa eneo la hospitali hiyo.
Awali, Mhandisi wa Idara ya Miundombinu ya Mkoa wa Morogoro, George
Tarimo alisema katika Mwaka wa Fedha wa 2016/2017, Serikali mkoani humo
kwenye bajeti ya maendeleo ya Mwaka wa Fedha wa 2016/2017, ilitenga Sh
milioni 108.2 kwa ajili ya ukarabati huo.
Tarimo alisema ukarabati huo unasimamiwa na mshauri mwelezi na
mkandarasi mkuu Ofisi ya Meneja wa Mkoa wa Wakala wa Majengo na ulianza
Aprili 5, mwaka huu na kutakiwa kukamilishwa ifikapo leo. Alisema hadi
sasa gharama za ujenzi ya awali ni Sh 89,602,993 na kwamba kiwango cha
kazi zilizokamilika kimefikia asilimia 65. Alisema hiyo inatokana na
nafasi finyu ya utendaji. Alifahamisha kuwa, jokofu lenye uwezo wa
kuhifadhi miili 18 limenunuliwa na bado lipo Bohari kuu ya Dawa (MSD).
CHANZO HABARI LEO
0 comments:
Post a Comment