Home » » RC MOROGORO AZUIA NAFAKA KUTUMIKA KUTENGENEZEA POMBE

RC MOROGORO AZUIA NAFAKA KUTUMIKA KUTENGENEZEA POMBE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

MKUU wa mkoa wa Morogoro, Dk Kebwe Stephen, amepiga marufuku wananchi hususani wakulima kutumia nafaka za chakula kutengenezea pombe kwa ajili ya sherehe za ngoma 'vigodoro', badala yake wahifadhi kwa matumizi ya chakula katika kaya zao.
Dk Kebwe alipiga marufuku mtumizi ya nafaka za chakula kutengenezea pombe katika ziara yake aliyoifanya hivi karibuni wilayani Kilosa kukagua shughuli za maendeleo.
Alisema utabiri wa Mamlaka ya Hali ya Hewa siku za hivi karibuni umeonesha kuwepo uwezekano kukosekana mvua za kutosha maeneo mbalimbali nchini, ukiwemo mkoa wa Morogoro.
Mkuu wa mkoa alitumia fursa hiyo kwenye mikutano ya hadhara ya wananchi wa vijiji vya Ulaya, Zombo na Kivungu wilayani humo kuwataka wahifadhi chakula kidogo kinachopatikana, badala ya kukiuza chote na fedha zake kutumia kucheza ngoma na kupika pombe.
“Agizo hili ni kwa wilaya za mkoa mzima, kuanzia sasa ni marufuku kwa mwananchi ama mkulima kuuza chakula chake chote kupata fedha za kuchezea ngoma na kutengeneza pombe, wale watakaobainika wachukuliwe hatua za kisheria," alisema.
Alisema hali ya mvua si nzuri na kuwataka wananchi hususani wakulima kukitumia vyema chakula walichonacho, hivyo aliwataka watendaji wa halmashauri za wilaya, kata, vijiji, tarafa na wakuu wa wilaya za mkoa huo kuanza kulisimamia kikamilifu agizo hilo.
Mkuu huyo wa mkoa aliwataka wananchi na wakulima katika wilaya za mkoa huo kulima mazao yanayokomaa haraka kwa kutumia mvua kidogo zinazonyesha, kuendeleza kilimo cha umwagiliaji maeneo yenye skimu za umwagiliaji ili kuongeza kiwango cha uzalishaji wa nafaka za mazao ya chakula.
Mkuu wa wilaya ya Kilosa, Adam Mgoyi, alisema hali ya chakula kwa mwaka 2015/2016 halmashauri ilizalisha tani 123,128 za nafaka , wakati mahitaji ya chakula cha nafaka kwa wilaya ni tani 103,957 na kwa takwimu hizo wilaya bado inajitosheleza kwa chakula msimu wa 2015/2016.
Hata hivyo, alisema kuna baadhi ya maeneo yameanza kuonesha upungufu wa chakula ambayo ni Magole, Kitete, Dumila, Maguha, Magumbike, Mamboya, Mtumbatu, Mabula na Kidete.
Mkuu huyo wa wilaya alitaja sababu kubwa ni kukatika kwa mvua mapema kulikosababisha mazao hasa mahindi kutokomaa vizuri.
Hata hivyo, alitaja mikakati ya wilaya katika kutatua kero ya sekta ya kilimo ni kuendelea kutoa elimu juu ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, kwa kuwafundisha wananchi kulima

CHANZO GAZETI LA HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa