Home » » ‘Acheni kufanya kazi kwa mazoea’

‘Acheni kufanya kazi kwa mazoea’

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango
WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango, amewataka wafanyakazi wa wizara hiyo kuacha kufanya kazi kwa mazoea.
Badala yake, waisaidie serikali kutimiza malengo yake ya kukusanya kodi ipasavyo na kudhibiti matumizi yasiyo na tija kuharakisha maendeleo ya nchi.
Aidha akizungumzia bajeti ya wizara inayotarajiwa kuwasilishwa bungeni wiki hii, Waziri Mpango alisema matumizi ya kawaida yamepunguzwa na fedha nyingi zimeelekezwa kwenye miradi ya maendeleo.
Dk Mpango alisema hayo hivi karibuni mjini Morogoro, wakati akizindua baraza jipya la wafanyakazi wa wizara hiyo mjini Morogoro.
Alisema jukumu kubwa la wizara hiyo ni kukusanya mapato na kuyasimamia. Aliomba ushirikiano kutoka kwa wafanyakazi wote wa wizara hiyo, watimize wajibu wao kufikia malengo hayo.
Aliwataka wataalamu hao kuhakikisha kuwa sera zinazotungwa zinakuwa rafiki na hazibadiliki mara kwa mara ili kuvutia uwekezaji na wawekezaji nchini.
Chanzo Gazeti La Habari Leo

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa