Mwenyekiti
wa Chama cha Mapinduzi CCM Dr. Jakaya Kikwete akizungumza katika
mkutano wa kumnadi mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.
John Pombe Magufuli uliofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri katika Manispaa
ya Morogoro mkoani humo ambapo maelfu ya wananchi mjini Morogoro
wamehudhuria katika mkutano huo.
Dr. John Pombe Magufuli amewaomba wananchi hao kumpigia kura za ndiyo
ifikapo Oktoba 25 mwaka huu na kumchagua ili aweze kuwatumikia
watanzania kwa ujumla wake na kushirikiana na wananchi katika kuleta
maendeleo ya watanzania ili kuipaisha Tanzania katika maendeleo.
Ameongeza
kwamba yeye atakuwa rais wa watanzania wote bila kujali itikadi zao za
vyama, Makabila, Dini wala Ukanda kwani maendeleo hayana vyama, Kabila,
Dini wala Ukanda ila ni kwa watanzania wote.(PICHA NA JOHN
BUKUKU-FULLSHANGWE-MOROGORO)
Mwenyekiti
wa Chama cha Mapinduzi CCM Dr. Jakaya Kikwete akisalimiana na mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli wakati
alipowasili kwenye uwanja wa jamhuri kwa ajili ya mkutano wa kampeni.
Mwenyekiti
wa Chama cha Mapinduzi CCM Dr. Jakaya Kikwete na Mgombea Urais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli wakiwapungia
mikono wananchi huku wakiwa wameshika kofia zao.
Mwenyekiti
wa Chama cha Mapinduzi CCM Dr. Jakaya Kikwete na Mgombea Urais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli wakifuatilia
jambo huku wakiwa na sura za tabasam wakati Mzee Yusuf Makamba
akihutubia wananchi mkoani Morogoro kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa
Morogoro Bw. Innocent Kalogeres.
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli
akiwahutubia wananchi wa mkoani Morogoro na kuomba kura kwenye mkutano
uliofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani humo.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli akisistiza jambo katika mkutano huo.
Maelfu ya wananchi wakiwa katika mkutano huo uliofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli
akimnadi Mgombea ubunge wa jimbo la Morogoro mjini Mh. Mohamed Abood.
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli
akimkabidhi ilani ya Uchaguzi mgombea ubunge wa jimbo la Morogoro mjini
Mh. Mohamed Abood.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa CCM Ndugu Abdallah Bulembo akiwahutubia wananchi wa Morogoro katika mkutano huo.
Mwenyekiti
wa Chama cha Mapinduzi CCM Dr. Jakaya Kikwete na Mgombea Urais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli wakiimba wimbo
katika mkutano huo kulia ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na kushoto ni
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Morogoro Bw. Innocent Kalogeres.
Msanii Ali Kiba akifanya vitu vyake jukwaani katika mkutano huo.
Kundi la muziki la TOT likitumbuiza katika mkutano huo.
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli
akipunga mikono kwa wananchi waliofurika katika uwanja wa Jamhuri mjini
Morogoro wakati akiwasili uwanjani hapo.
Baadhi
ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe wakimpokea Mgombea Urais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli wakati akielekea
mjini Morogoro.
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli
akizungumza na wananchi akiwa njiani kutoka Ifakara kwenda Kilosa mkoani
humo.
Baadhi
ya watoto wakiwa wameshikilia picha ya Mgombea Urais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli wakati wa mkutano wa
kampeni mjini Kilosa.
Baadhi
ya Watawa wakifurahia jambo wakati Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli akizungumza mjini Mikumi.
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli
akimnadi mgombea ubunge wa jimbo la Mlimba Bw.Godwin Emmanuel Kunambi.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli akimnadi mgombeaJonas Estomih Nkya.
Mmoja wa wananchi waliojitokeza katika mkutano huo akifurahia jambo.
Wananchi wa Kilombera wakinyanyua mabango yao juu juu wakati wa mkutano huo.
"Hapa ni Kazi tu"
Steven Nyerere anakamua tu hapo.
0 comments:
Post a Comment