Home » » DK MAGUFULI KUWANYANG'ANYA VIGOGO ARDHI WALIYOJILIMBIKIZIA ATAIGAWA KWA WANANCHI‏

DK MAGUFULI KUWANYANG'ANYA VIGOGO ARDHI WALIYOJILIMBIKIZIA ATAIGAWA KWA WANANCHI‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli akikimbia kuonesha ukakamavu kwenda jukwaani kujinadi wakati wa mkutano wa kampemi  katika Uwanja wa Taifa mjini Ifakara wilayani Kilombero, Mkoa wa Morogoro leo. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akijinadi kwa wananchi katika mkutano wa kampeni uliofanyika Mjini Ifakara, wilayani Kilombero, Morogoro. Dk Magufuli jana alifanya pia kampeni katika wilaya za Ulanga na Malinyi.

Akihutubia kwa nyakati tofauti katika Wilaya za Ulanga, Malinyi na Kilombero, Dk Magufuli amesema kuwa akipta ushindi atawanyang'anya ardhi vigogo wote waliojilimbikizia ardhi bila kujiendeleza na kuigawa kwa wakulima na wafugaji nchini.
 Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akijinadi akifanananisha upara wake na wa Mgombea Ubunge wa Jimbo jipya la Malinyi katika mkutano wa kampeni uliofanyika jana katika Kata ya Mtimbila Wilaya mpya ya Malinyi, Morogoro. Dk Magufuli  alifanya pia kampeni katika wilaya za Ulanga na Kilombero
 Mmoja wa wananchi akiwa na bango linalosema Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli anasubiri kuapishwa tu katika mkutano wa kampeni uliofanyika jana Mjini Ifakara, wilayani Kilombero, Morogoro. Dk Magufuli alifanya pia kampeni katika wilaya za Ulanga na Malinyi.
 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akikagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Kilombero alipokuwa akitoka kufanya kampeni katika Wilaya za Ulanga na Malinyi kwenda   Mjini Ifakara, wilayani Kilombero, Morogoro.
 Mmoja wa wafuasi wa CCM akiwa na picha ya Dk Magufuli mjini Mahenge, wilayani Ulanga
 Wananchi wakishangilia baada ya kufurahishwa na hotuba ya Dk Magufuli mjini Mahenge, Ulanga
 Madini wakinadiwa na Dk Magufuli wakati wa mkutano wa kampeni mjini Mahenge leo
 Dk Magufuli akiombewa na mmoja wa masheikh baada ya kumaliza kujinadi kwa wananchi mjini Mahenge Ulanga
 Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akimpatia zawadi mtoto alipokuwa akiondoka mjini Mahenge wilayani Ulanga, baada ya kufanya mkutano wa kampeni
 Wananchi waliouzuia msafara wa Dk Magufuli katika Kijiji cha Ilagua Mission, Wilaya mpya ya Malinyi ukielekea Kata ya Mtimbila.
 Moja ya mabango yaliyishikwa na wananchi katika mkutano wa kampeni katika Kata ya Mtimbila, wilayani Malinyi leo
 Wananchi wakishangilia wakati Dk Magufuli akiwasili kwenye mkutano wa kampeni katika Kata ya Mtimbila
 Dk Magufuli akijinadi kwa wananchi katika Kata ya Mtimbila, wilayani Malinyi
 Mwananchi akitafakari wakati Dk Magufuli akihutubia na kutoa ahadi ikiwemo ya kuanzisha malipo ya pensheni kwa wazee nchini
 Hureee Dk Magufuli
 Dk Magufuli akimnadi Mgombea ubunge Jimbo la Malinyi, Dk. Harji Mponda wakati wa mkutano huo
 Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Ulanga, mkoani Morogoro, Said Kitila akitangaza kukihama chama hicho na kujiunga na CCM katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika Kata ya Mtimbila, wilaya mpya ya Malinyi, mkoani Mororogoro
 Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema wa Uratibu wa Msingi Wilaya ya Ulanga, Evance Tagala akionesha kadi kabla ya kuikabidhi kwa Dk Magufuli alipotangaza kukihama chama hicho na kujiunga na CCM wakati wa mkutano huo wa kampeni katika Kata ya Mtimbila.
 Tagala akipongezwa na wafuasi wa CCM baada ya kujiunga na chama hicho
 Wananchi wakimsikiliza Dk Magufuli alipokuwa akijinadi katika Kijiji cha Lupilo wilayani Ulanga
 Kijana akiwa na uso wa mshangao baada ya kumuona Dk Magufuli alipokuwa akizungumza na wananchi kabla ya kuvuka Mto Kilombero akitokea wilayani Ulanga kwenda Ifakara
 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akikagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Kilombero alipokuwa akitoka kufanya kampeni katika Wilaya za Ulanga na Malinyi kwenda   Mjini Ifakara, wilayani Kilombero, Morogoro.



 Mmoja wa wananchi akiwa na bango linalosema Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli anasubiri kuapishwa tu katika mkutano wa kampeni uliofanyika jana Mjini Ifakara, wilayani Kilombero, Morogoro. Dk Magufuli alifanya pia kampeni katika wilaya za Ulanga na Malinyi.  (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
 Ni furaha iliyoje kwa mwananchi huyu
 Sehemu ya umati wa watu wakati wa kampeni CCM kwenye Uwanja wa Taifa, Ifakara wilayani Kilombero, Morogoro , uliohutubiwa na Mgombea urais wa CCM, Dk John Maguful
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazee wa CCM, Abdalah Bulembo  akizungumza maneno ya kumnadi Dk Magufuli kabla ya kumkaribisha kujinadi wakati wa mkutano wa kampeni mjini Ifaraka

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa