Hofu
imeendelea kutanda kwa wafungaji mkoani Morogoro kufuatia bodaboda
kuendelea kuwavamia na kuwapora wafugaji kila wanapoonekana katika mji
wa Morogoro kwa madai ya kulipiza kisasi baada ya mkulima mmoja kuuwawa
katika bonde la mgongola ambapo wafanyabiashara wafugaji na wanaofanya
shughuli za ulinzi wamelazimika kuukimbia mji wa Morogoro na baadhi
ya wanafunzi wa vyuo na kurudi majumbani.
Wakizungumza wakiwa porini kujadili hatma ya usalama wa wafugaji
hao wakiwemo wanaume kwa wanawake kutoka wilaya za Kilosa na Mvomero
wamesema hawakuusika na mgogoro uliosababisha mauaji ya mkulima katika
bonde la mgongola na hivyo kuomba serikali kupitia vyombo vya ulinzi na
usalama wawasaidie kwani hivi sasa wagonjwa wanalazimika kutibiwa
majumbani wanafunzi hawaendi shule kwa kuhofia madereva wa bodaboda.
Nao baadhi ya wafugaji waliojeruhiwa na kuporwa fedha wameeleza
jinsi walivyovamiwa na kupigwa kisha kunyanganywa simu na fedha na hivi
sasa wanaugulia majumbani na wanashindwa kwenda hospitali kupata
matibabu kwa hofu ya kuvamiwa na madereva wa bodaboda huku baadhi ya
wanafunzi wafugaji wanaosoma chuo cha St Josefu Morogoro nao wameelezwa
kurudi majumbani.
Wakati haya yakitokea jeshi la polisi mkoa wa Morogoro
limewafikisha mahakamani madereva wa boda boda 11 waliobainika kuhusika
na matukio ya kuvamia wafugaji ambapo wamesomewa mashataka mawili ya
kuvamia wafugaji kwanyakati tofauti mbele ya hakimu mkazi Maua Hamduni
ambapo washtakiwa wamenyimwa dhamana kwa hofu ya usalama wao na
kurudishwa rumande .
KUELEKEA UCHAGUZI 2015: JE UNAPENDA NANI AWE KIONGOZI WAKO? JAZA FOMU HII FUPI HAPA
0 comments:
Post a Comment