Home » » VIJANA WATAKIWA KUJIKITA KATIKA SHUGHULI ZA KILIMO

VIJANA WATAKIWA KUJIKITA KATIKA SHUGHULI ZA KILIMO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 

WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Sophia Simba amewashauri vijana nchini kujikita katika shughuli za kilimo ili waweze kujiajiri wenyewe na kuinua kipato chao badala ya kukaa vijiweni.

Hayo alisemwa jana wakati akikagu baadhi ya mabanda na vipando vilivyopo katika uwanja wa maonesho ya kilimo ya Julius Kambarage Nyerere mjini Morogoro.

Simba alisema kuwa wakati sasa umefika kwa vijana kuacha kukaa vijiweni ama kuilalamikia serikali kuhusu kukosa ajira na badala yake wajiunge kwa pamoja katika kufanya shughuli za kilimo na ufugaji, kwani kilimo ndio ajira mama hapa nchini.

"Nawahimiza vijana wote kuacha tabia ya kutopenda kujishughulisha na kubaki kulalama kuwa serikali haijawapatia ajira, kwani wanayo fursa kubwa ya kujikwamua kiuchumi, endapo watajikita kikamilifu kwenye kilimo.

Aidha aliwataka washiriki wa maonesho ya wakulima kuhakikisha wanalima kilimo chenye ubora wakisaidiwa kikamilifu na maofisa ugani katika kuwapatia mbinu bora za kilimo.

Katika hatua nyingine, aliwakemea baadhi ya maofisa ugani wasio waadilifu na wanaowatoza fedha wakulima pindi wanapohitaji kuhudumiwa ama kupata ushauri wa kitaalamu katika kilimo, kwani ni kinyume na sheria na maadili ya kazi.

"Nakemea vikali baadhi ya maofisa wa kilimo wanaodai fedha kwa wakulima ama wafugaji wetu ili kutoa huduma," alisema.

Kwa upande wake mjumbe wa kamati ya uratibu Kanda ya Mashariki Yahya Kijoli aliishauri wizara hiyo kuweka mpango maalumu wa kuwabadilisha vijana kimtazamo hasa suala la ajira, kwani wengi wao wamekuwa hawajishughulishi.

"Tunaiomba serikali ielekeze zaidi katika kuunda mfumo utakowabadilisha vijana kimtazamo ili wapende kilimo kwani wamekuwa wakiona kilimo kuwa ni cha watu wasio wasomi,"alisema.

Hata hivyo waziri alisema ili vijana wabadilike mtizamo ni lazima mabadiliko hayo yaanzie ngazi ya familia, kata, vijiji na hata vitongoji kwani serikali haiwezi kujenga utaratibu kwa nchi nzima bali kupitia ngazi kuu ya serikali ni kuweka mazingira mazuri kwa hayo ambayo vijana wanataka kutekelezwa

Chanzo:Majira

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa