Home » » MORO TALENT YATUNUKU WAANDISHI

MORO TALENT YATUNUKU WAANDISHI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
KITUO cha kuibua na kukuza vipaji vya wasanii mkoani hapa, Moro Talent, kimewatunuku tuzo maalumu za umahiri wa habari za kijamii 2014 waandishi mbalimbali akiwamo Joseph Malembeka wa gazeti hili.
Sambamba na Malembeka kupokea tuzo hiyo iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera, mwishoni mwa wiki, pia viongozi wa umma na binafsi katika ngazi mbalimbali, wafanyabiashara, wasanii na wadau mbalimbali walitunukiwa.
Wengine waliotunukiwa ni Mwenyekiti wa klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Morogoro (MOROPC), Idda Mushi, Mratibu MOROPC Thadei Hafigwa, John Nditi na Prince Baina Kamukulu.
Kabla ya kutolewa tuzo hizo, Mratibu wa Moro Talent Award, Mohamed Ngwenje, alisema uamuzi huo umetokana na agizo la mkuu wa mkoa huyo mwaka jana, kukitaka kituo hicho kutambua kazi za wasanii na kuzitangaza kwa nguvu zaidi.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa