Home » » WANAKIJIJI WAVAMIA SHAMBA MOROGORO,WAGAWANA

WANAKIJIJI WAVAMIA SHAMBA MOROGORO,WAGAWANA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WAKAZI wa Kijiji cha Lubungo A, Kata ya Mikese, wilayani Morogoro, wamevamia shamba linalodaiwa kupewa mwekezaji kinyemela na uongozi wa kijiji wakishirikiana na wilaya na kugawiana kisha kukesha wakifyeka msitu.
Uvamizi huo unaohusisha eneo hilo linalokadiriwa kuwa na ukubwa wa ekari 1,000 unatokana na wanakijiji hao kubaini kuwa eneo hilo ambalo hawajawahi kulipangia matumizi linakodishwa kwa watu wengine.
Wakizungumza kwa nyakati toafuti, Shabani Salumu, Ester Daud na Hussein Mzuri, walisema wamechoshwa na rushwa kwa viongozi wao na kuuza eneo lote kwa wawekezaji bila kuwashirikisha.
“Hapa kijijini tunakadiriwa kuwa zaidi ya watu 2,400 na tumezaliana hadi hatuna eneo la kutanulia kijiji kwa shughuli za maendeleo na uzalishaji, leo eneo linauzwa kinyemela, sisi na vizazi vyetu twende wapi?” alihoji Salumu.
Kwa upande wake, Ester alisema viongozi wamekuwa wabadhirifu wa ardhi.
Mwenyekiti wa kijiji hicho, Juma Mgunda mbali na kukiri kuwepo ongezeko la wananchi kijijini hapo na eneo kupungua, alikanusha kuuza eneo hilo huku akiutupia lawama uongozi uliopita.
“Eneo lenye mzozo kwa mujibu wa kumbukumbu zangu linaonyesha ni mali ya padri ambaye naambiwa anaitwa Father Seti na alilipata mwaka 1996 akiwa na lengo la kujenga chuo, ili watoto wanaohitimu katika maeneo yetu wapate ujuzi,” alisema Mgunda.
Alisema ingawa wananchi hao wamevamia, lakini hawakupaswa kufanya hivyo.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa