Home » » BENDERA KUWASHUGHULIKIA WATUMISHI WAZEMBE

BENDERA KUWASHUGHULIKIA WATUMISHI WAZEMBE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera, amewaagiza wakurugenzi wa wilaya mkoani hapa kupeleka haraka taarifa za watumishi wazembe na wasio waadilifu ofisini kwake, ili awachukulie hatua za kisheria.
Bendera alitoa agizo hilo mjini hapa juzi katika kikao cha madiwani wa Halmashauri ya Morogoro cha kupitia majibu ya hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (GAG) mwaka 2012/ 2013.
“Muda wa kuleana umepita, nileteeni majina ya watu wasiowajibika na wasio na uadilifu niwashugulikie… ni aibu kuwa na lundo la watu eti watumishi ofisini wakati ufanisi wake ni ziro,” alisisitiza Bendera.
Alitoa kauli hiyo baada ya kusoma taarifa ya CAG ambayo imeonyesha mkoa huo kufanya vizuri katika hesabu zake, hususani katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na mamlaka za serikali za mitaa na kupata hati safi kwa mwaka 2012/2013.
Pamoja na mkoa kupata hati safi, Bendera aliwataka watumishi wake kutoridhika na mafanikio hayo na badala yake waendelee kupambana, ili kudumisha mafanikio kwa lengo la kufikia kiwango cha juu kabisa.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa