Home » » WAJASIRIAMALI WATAKIWA KUTUMIA FURSA ZA MIRADI

WAJASIRIAMALI WATAKIWA KUTUMIA FURSA ZA MIRADI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Wafanyabiashara wakichambua vitunguu katika soko ya vitunguu la Misuna mjini Singida baada ya msimu wa kuvuna na kuuza vitunguu kuanza. Gunia moja linauzwa kwa bei ya sh120,000

Wajasiriamali katika Manispaa ya Morogoro, wameshauriwa kutumia fursa zilizopo katika Mradi wa Uhusiano wa Maendeleo ya Kiuchumi (MPED), ili kuboresha vipato vyao.
Mwezeshaji wa Mkusanyiko wa Wajasiriamali wa Manispaa ya Morogoro, Martina Pangani, alisema mradi huo umeanzishwa kwa ushirikiano wa manispaa na mji wa Kitchener, nchini Canada.
Alisema mradi huo ni wa manufaa kwa wajasiriamali na kwa msingi huo kuna haja ya watu kujitokeza na kutumia fursa hizo kikamilifu.
Hata hivyo, alieleza masikitiko yake kuhusu wajasiriamali kucheleweshewa vibali vya kusambaza bidhaa zao ndani na nje ya nchi, jambo linalowakatisha tamaa. Pangani aliliomba Shirika la Viwango Tanzania (TBS), kujenga utamaduni wa kukagua bidhaa za wajasiriamali hao na kutoa vibali kwa haraka.
Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Mkusanyiko huo, Ibrahim Sanane, alisema mkusanyiko huo utawasaidia wajasiriamali kubadilishana uzoefu kuhusu kutengeneza bidhaa bora.
Sanane alisema wajasiriamali wengi nchini wanakabiliwa na tatizo la kukosa masoko, jambo linalowalazimisha kuzalisha bidhaa kwa kiwango kidogo.
Wajasiriamali wanaounda mkusanyiko huo ni wa sekta za usagishaji wa nafaka, utalii, ufugaji kuku, mbao, nguo na nyama.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa