Home » » Apex wataka ripoti ya CAG

Apex wataka ripoti ya CAG

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WAFANYAKAZI wa Chama Kilele cha Wakulima wa Tumbaku Tanzania (Apex), wamemtaka Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) kuweka hadharani taarifa ya ukaguzi wa chama hicho kutokana na kuibuka madai kuwa kimefuja sh bilioni 16.
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Mashambani na Kilimo Tanzania (TPAWU) – Apex, Leonard Maganga, alisema wafanyakazi hao wanaomba ripoti hiyo ili kuwaondolea hofu inayowakabili juu ya hatima ya chama hicho kutokana na Bunge lililopita kutaka kifutwe kwa kinachodaiwa kuwa na ubadhirifu.
“Hadi sasa tuna takribani miezi tisa tangu ufanyike ukaguzi ofisini kwetu juu ya tuhuma na madai yaliyoorodheshwa na wabunge juu ya Apex, lakini hakuna mrejesho… tunataka kujua hatima ili wafanyakazi tuwe na uamuzi,” alisema Maganga.
Katika ufafanuzi wake, mwenyekiti huyo alisema wafanyakazi wa chama hicho wanashangazwa na mswada wa Waziri wa Chakula la Ushirika, Christopher Chiza, kukifuta wakati kuna vyama kikiwemo kinachowaunganisha wanunuzi wa zao hilo (ATTT) ni chanzo cha kumdhulumu mkulima pato lake.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa