Home » » Wataalamu watakiwa kuhamasisha ufugaji nyuki

Wataalamu watakiwa kuhamasisha ufugaji nyuki

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

MKUU wa Wilaya ya Gairo mkoani Morogoro, Bi.Khanifa Karamagi amewataka wataalamu wa misitu wilayani humo kuhamasisha wananchi kuanzisha vikundi vya ufugaji nyuki na kuhakikisha vimesajiliwa kisheria ili viweze kupata misaada kutoka serikalini.
Bi.Kharamagi aliyasema hayo katika maadhimisho ya siku ya utundikaji mizinga kitaifa ambapo kimkoa ilifanyika wilayani humo.
Alisema kuwa kuhamasisha uanzishaji wa vikundi vya ufugaji nyuki na kuhakikisha vimesajiliwa kisheria ni jambo la msingi katika kuvutia wawekezaji na kuweza kupatiwa misaada kutoka serikalini na taasisi mbalimbali.
Pia alisema kuwa rasilimali misitu na nyuki vikiendelezwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho na kuhamasisha ufugaji nyuki kwa jamii na utunzaji wa misitu ili kuongeza mazao ya nyuki kama asali, nta na gundi.
Aidha aliwataka wataalamu wa misitu kuhamasisha watu binafsi kuwa na mizinga ya kisasa ili kupata mavuno bora na mengi yatokanayo na mazao ya nyuki.
Kwa upande wake Meneja wa misitu Wilayani humo, Bw.Abdin Mrema alimweleza mkuu huyo kuwa wananchi wengi wilayani humo bado hawajahamasika kufuga nyuki pamoja na elimu ya ufahamu kutolewa lakini inaonekana waliopata elimu hii ni wachache,hivyo inabidi juhudi za uhamasishaji ziongezeke.
Katika maadhimisho hayo zaidi ya vikundi kumi na moja vilijitokeza na kupatiwa mizinga ya kisasa na zaidi ya mizinga arobaini ilitundikwa katika msitu wa Msingisi.
Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni Boresha ufugaji nyuki linda ubora wa mazao yake.

Chanzo;Majira

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa