Home » » WAHANGA WA MAFURIKO DUMILA WAKOSA MAKAZI

WAHANGA WA MAFURIKO DUMILA WAKOSA MAKAZI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WAHANGA wa mafuriko katika maeneo ya Dumila, mkoani Morogoro wanakabiliwa na hali ngumu ya ukosefu wa makazi  baada ya nyumba zao za muda (mahema) kuezuliwa na kimbunga kilichoambatana na mvua.
Akizungumza na Tanzania Daima Jumapili kwa njia ya simu,  Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mateteni Dumila, Iddi Mangilile, alisema mvua hizo zimechangia kuharibika kwa mahema hayo.
Mangilile alisema mvua ilianza kunyesha nyakati za mchana na kusababisha ukosefu wa makazi huku familia nyingi zikiishi kwa kutangatanga.
Alisema licha ya Chama cha Msalaba Mwekundu kukarabati mahema hayo bado wapo katika hali ngumu kwani familia nyingi zimeshindwa kuendelea kujishughulisha kama ilivyokuwa awali.
“Tunashukuru sana Chama cha Msalaba Mwekundu kuwa nasi bega kwa bega kipindi chote cha matatizo ya mafuriko hadi sasa kwani mvua bado zinaendelea kunyesha na zinaambatana na upepo mkali, hivyo bado tupo katika wakati mgumu,” alisema.
Naye Rais wa chama hicho, Dk. George Nangale, alisema wanashirikiana na serikali ili kuwapatia familia 400 maeneo ya kuishi ya muda kwa lengo la kujihifadhi katika kipindi hiki.
Alisema waliwapatia makazi hayo ya muda wakazi wa vijiji hivyo ambayo yalijengwa kwa ustadi lakini mvua iliyoambatana na upepo iliyonyesha juzi ilichangia kuezuliwa kwa nyumba hizo.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by : Tone Media
Copyright © 2012. Morogoro Yetu - All Rights Reserved
Template Modify by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa